Header Ads Widget

MSAFARA WA MPINA WAZUIWA KUINGIA OFISI ZA INEC



Msafara wa mgombea wa Urais kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Mpina, umekumbana na kizuizi cha kuingia katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) mjini Dodoma leo, wakati wagombea kutoka vyama mbalimbali walipofika kurejesha fomu zao.

Mpina, ambaye hivi karibuni alihama kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) baada ya kushindwa katika kura za maoni za ubunge Jimbo la Kisesa, alijiunga na ACT Wazalendo na kuomba kugombea nafasi ya urais kupitia chama hicho.


Hata hivyo, uamuzi wa chama hicho kumteua umeibua mtazamo tofauti ndani na nje ya chama, baada ya Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya ACT Wazalendo, Monalisa Ndala, kupinga uteuzi huo akidai kanuni za chama zimekiukwa. Katika barua aliyomwandikia Katibu Mkuu wa chama, Ado Shaibu, Monalisa alieleza kuwa Mpina hajakidhi kanuni za kudumu za chama toleo la mwaka 2015, hususan kanuni namba 16 (4) (iv) inayomuhitaji kuelewa itikadi, falsafa, misingi na sera za chama.


Kutokana na pingamizi hilo, Siku ya jana Mkurugenzi wa Uchaguzi wa INEC, Ramadhan Kailima, alimwandikia barua Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo akieleza kuwa tume hiyo, kupitia barua yake ya awali ya Agosti 15, 2025, ilieleza kuwa Mpina hatapaswa kufika katika Ofisi za Tume kwa ajili ya uteuzi uliopangwa kufanyika Agosti 27, 2025.


Baada ya barua hiyo, ACT Wazalendo ilitoa taarifa ikipinga uamuzi wa Msajili wa Vyama vya Siasa wa kutengua uteuzi wa Mpina, ikieleza kuwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa chama inaendelea kupitia hatua hiyo kwa umakini na itatoa mwelekeo wake wa kina katika muda muafaka.

 


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI