Header Ads Widget

MIILI MITANO YAFUKULIWA KARIBU NA SHAKAHOLA

 

Miili mitano imegunduliwa huko Kilifi kufuatia kumalizika kwa makaburi 6 katika kijiji cha Kwa Binzaro karibu na Shakahola katika mkoa wa pwani wa Kenya.

Hii inakuja baada ya ugunduzi wa makaburi yenye kuhusishwa na kanisa la ‘Kufunga hadi Kufa’ huko Shakahola lililosababisha vifo vya watu zaidi ya 400 mnamo 2023.

Hussein Khalid, mwanaharakati wa haki za binadamu na Mkurugenzi Mtendaji wa Vocal Africa ambaye alikuwa kwenye maeneo ya makaburi alisema:

"Mwili wa kwanza ambao ulipatikana na wenyewe ulionekana kuzikwa hapo hivi karibuni wiki mbili hadi tatu zilizopita. Lakini minne inaonekana kuwa ilizikwa kitambo kidogo na ilikuwa katika hali ya kuharibika."

Makaburi 21 yanatarajiwa kufukuliwa hii leo.

Kwa mujibu wa Bwana Khalid, kuchimbwa kwa kaburi la kwanza jana kulionyesha dalili za mchezo fulani unaoendelea.

"Hakuna mabaki yaliopatikana lakini ilionekana kana kwamba siku zilizopita, mtu, watu wengine au kundi fulani waliondoa maiti zilizokuwepo hapo. Ishara zilionyesha wazi kwamba kulikuwa na mwili eneo husika. Kitu pekee ambacho tulipata kutoka kaburi la kwanza kilikuwa nguo za ndani za wanawake na watoto. Hiyo ilionyesha kwamba inawezekana mtu au watu waliozikwa hapo walikuwa wanawake na watoto."

Hayo yanajitokeza baada ya hofu kwamba ‘Kanisa la Kufunga hadi Kufa’ huenda nado linaendeleza shughuli zake licha ya Mchungaji wake Paul Mackenzie kuwa kuzuizini.

Mwezi uliopita, mahakama ya Kenya ilikuwa imeamuru kufukuliwa kwa miili inayoshukiwa kuwa ni ya watu ambao walikufa kwa njaa na kukosa hewa kaunti hiyo hiyo ambapo mamia ya washiriki wa kanisa la Mackenzie walipatikana miaka miwili iliyopita.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI