Header Ads Widget

ISRAELI KUANZA MAZUNGUMZO YA KUWAACHILIA MATEKA WOTE NETANYAHU ASEMA

 

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema ameagiza kuanza kwa mazungumzo ya kuachiliwa kwa mateka wote waliosalia na kukomesha vita huko Gaza kwa masharti "yanayokubalika na Israel".

Netanyahu aliwaambia wanajeshi wa Israel Alhamisi usiku kwamba baraza lake la mawaziri pia limeidhinisha mipango ya shambulio kubwa katika mji wa Gaza kaskazini mwa eneo hilo, licha ya upinzani mkubwa wa kimataifa na wa ndani.

Hamas ilikubali pendekezo lililotolewa na wapatanishi wa Qatar na Misri kwa ajili ya kusitisha mapigano kwa siku 60 siku ya Jumatatu, ambayo kwa mujibu wa Qatar itashuhudia kuachiliwa kwa nusu ya mateka waliosalia huko Gaza.

Lakini akijibu kwa mara ya kwanza, Netanyahu hajakubali mpango huo uliopo mezani kwa sasa.

Vyombo vya habari vya Israel vimemnukuu afisa wa Israel akisema wapatanishi watatumwa kwa mazungumzo mapya pindi eneo litakapoamuliwa.

Katika taarifa yake ya video alipotembelea makao makuu ya kitengo cha Gaza nchini Israel Alhamisi usiku, Netanyahu alisema "ameagiza kuanza mara moja mazungumzo ya kuachiliwa kwa mateka wetu wote".

"Nimekuja kuidhinisha mipango ya IDF (Vikosi vya Ulinzi vya Israel) kuchukua udhibiti wa Mji wa Gaza na kuwashinda Hamas," alisema.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI