Header Ads Widget

IRAN YAFANYA ZOEZI LA KWANZA LA KIJESHI TANGU VITA YA SIKU 12 YA ISRAEL


Jeshi la Wanamaji la Iran linasema lilitumia makombora matatu ya baharini, yaliyopewa jina la "Nasir, Ghadir, na Ghader," katika mazoezi ya kombora ya "Eqtdar Paydar 1404".

Haya ni mazoezi ya kwanza ya kijeshi kwa Iran tangu vita vya siku 12 na Israel.

Kwa mujibu wa tangazo la Jeshi la Wanamaji la Iran, zoezi hili la kombora lilianza (Alhamisi, Agosti 21) kwa lengo la kuonyesha "nguvu ya ulinzi na kujaribu silaha za hivi karibuni" kaskazini mwa Bahari ya Hindi na Bahari ya Oman, na "vitengo vya ardhini, vitengo vya kuruka, maeneo ya makombora ya ufuo wa Bahari na wengineo".

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa ya Iran, wakati wa mazoezi hayo makombora na ndege zisizo na rubani yalirushwa kwenye shabaha katika maji ya Bahari ya Hindi.

Awali Admiral Abbas Hassani, msemaji wa zoezi hilo, alisema kwamba zoezi hilo litafanyika kwa siku mbili. Hata hivyo, idara ya mahusiano ya umma ya jeshi ilitangaza kuwa zoezi la kombora lilimalizika kwa "kufikia malengo yaliyopangwa mapema".

Zoezi hili la kombora lilifanyika takriban mwezi mmoja baada ya mazoezi ya pamoja ya Iran na Urusi, ambayo yalifanyika katika maji ya Bahari ya Caspian. 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI