Header Ads Widget

BOTSWANA YATANGAZA HALI YA DHARULA YA KITAIFA YA AFYA YA UMMA


 Botswana imetangaza hali ya dharura ya afya ya umma huku ikikabiliwa na uhaba wa dawa muhimu na vifaa vya matibabu.

Rais Duma Boko alitoa tangazo hilo katika hotuba aliyoitoa kupitia televisheni siku ya Jumatatu, akiweka mpango wa mamilioni ya pauni kurekebisha mlolongo wa mgawo wa huduma za afya utakaosimamiwa chini ya uangalizi wa kijeshi.

Kudhibiti uhaba huo litakuwa jambo "nyeti sana kwa bei kutokana na hazina yetu ndogo", aliliambia taifa.

Uchumi wa nchi hiyo umekumbwa na mdororo katika soko la kimataifa la almasi, kwani ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kwa uzalishaji wa almasi duniani.

Tatizo hili lililochochewa zaidi na upunguzaji wa misaada ya Marekani,limewaacha Wabotswana wengi kati ya raia 2.5m wakikabiliwa na ukosefu wa ajira na viwango vya juu vya umaskini, kulingana na ripoti za vyombo vya habari.

"Kazi hiyo itasalia bila kukoma hadi mlolongo mzima wa manunuzi utakapowekwa," Boko alisema katika hotuba yake, akitangaza kwamba wizara ya fedha imeidhinisha pula milioni 250 za Botswana (sawa na £13.8m) kwa ufadhili wa dharura.

Mapema mwezi huu, wizara ya afya ya nchi hiyo ilitoa tahadhari kwamba inakabiliwa na "changamoto kubwa", ikiwa ni pamoja na uhaba wa matibabu na madeni ya zaidi ya pula bilioni moja (£ 55.2m).

Sehemu kubwa ya madeni hayo yalitokana na wagonjwa kulazwa katika hospitali za kibinafsi kwa huduma ambazo hazikupatikana kwa umma.

Uhaba uliotajwa na Waziri wa Afya Dk Stephen Modise ni pamoja na ule wa dawa na vifaa vya kudhibiti saratani, matibabu ya VVU na kifua kikuu miongoni mwa mengine.

Kabla ya kupunguzwa kwa misaada ya Marekani iliyotolewa na Rais Donald Trump, Marekani ilifadhili theluthi moja ya udhamini wa VVU nchini Botswana, kulingana na UNAIDS .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI