Header Ads Widget

ARSENAL YAIPOKONYA TOTTENHAM HOTSPUR EBERECHI EZE MDOMONI

 

Hatua ya kushangaza ya Arsenal ya kumnyakua Eberechi Eze kutoka kwa mahasimu wao Tottenham Hotspur ni isiyo na huruma na kuonyesha huu ndio msimu ambao wamepanga kujinyakulia zawadi kubwa zaidi.

Spurs walikuwa tayari kuzindua zulia jekundu kumkaribisha mshambuliaji wa Crystal Palace wa Uingereza siku ya Jumatano, makubaliano hayo yalikamilika na dalili zote zilionyesha kwamba mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 alikuwa tayari kuhama.

Baadaye ilibainika kuwa Arsenal walikuwa wakitathmini jeraha la goti la mshambuliaji Kai Havertz, ambalo linaweza kuwatia doa katika safu yao ya mashambulizi - udhaifu ambao ulikuwa na athari kubwa katika kikosi cha kocha Mikel Arteta kumaliza akiwa mikono mitupu kwa mwaka wa tano mfululizo msimu uliopita.

Badala ya kwendea chaguo la gharama ya chini la kutafuta wa mkopo kama ilivyotarajiwa, Arsenal walijitokeza kwa mtindo wa aina yake kwa kuandaa pauni milioni 60 ili kumleta Eze Uwanja wa Emirates akiwa tu anakaribia kuingia mikononi mwa Spurs.

Uhamisho wa Eze kwenda Arsenal, ambao sasa unatarajiwa kukamilishwa kwa mafanikio, sio tu pigo kubwa la kisaikolojia lililolenga London kaskazini huko Spurs.

Ni ishara tosha kwamba hawana nia ya kubahatisha kwenye lengo lao la kujiimarisha katika kuwania taji la Ligi Kuu, pamoja na kujiweka sawa kwenye Ligi ya Mabingwa kwa mara nyingine tena baada ya kutinga nusu fainali msimu uliopita.

Ni mkakati tofauti kabisa wa kukabiliana na hali mbaya iliyoikumba Arsenal msimu uliopita, wakati kushindwa kwao kutatua tatizo lililo wazi - yaani kusajili mshambuliaji imara - kuliigharimu pakubwa.

Spurs walidhani walikuwa wameshamchukua Eze, uwezekano wa makubaliano ya pesa pamoja na Richarlison ulijadiliwa, lakini Arsenal walijitokeza kwa kasi kubwa mara tu walipokabiliwa na uwezekano wa Havertz kuachwa nje.

Arsenal wamekuwa wakihusishwa na Eze majira yote ya kiangazi, lakini ilifikiriwa kuwa nia yao ilikuwa imefifia mara Ethan Nwaneri alipokubali mkataba mpya wa miaka mitano, pamoja na kumsajili winga wa Chelsea Noni Madueke kwa mkataba wa £48.5m.

Jeraha la Havertz, na matokeo yake yanayoweza kutokea, yaliamsha hamu yao na kuwaacha Spurs wakiwa wameduwaa.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI