Header Ads Widget

FATUMA MWASSA,SI DHAMBI MTUMISHI WA UMMA KUWA MJASIRIAMALI.


Na Mariam Kagenda 

Matukio Daima Kagera

Watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Missenyi mkoani Kagera wamehimizwa kuanzisha miradi yao Binafsi kupitia mishahara wanayoipata ili kujiongezea kipato na kujikwamua kiuchumi . 

Mkuu wa mkoa wa Kagera  Hajjat Fatuma Mwassa amesema hayo wakati wa Tamasha la watumishi wa Halmashauri ya Missenyi ambalo liliambatana na michezo mbalimbali ikiwemo kuvuta kamba na Moira wa miguu likiwa na kauli mbiu isemayo "Mahusiano na afya bora kwa ustawi wa huduma bora kwa wananchi . Shiriki Uchaguzi mkuu Oktoba 2025 

Hajjat  Mwassa amesema kuwa si dhambi mtumishi wa umma kufanya shughuli za ujasiriamali ambazo zitamsaidia kujiongezea kipato kwani watumishi hao wanavyo vipawa mbalimbali hivyo Halmashauri itafute mashamba  watumishi waweze kulima na kufuga Jambo ambalo litawasaidia kuongeza kipato.

Ameongeza kwa kuipongeza halmashauri hiyo kwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo na kuwa kazi kubwa imefanyika katika Halmashauri hiyo kwenye utekelezaji wa miradi ili kutatua changamoto ambazo wananchi walikuwa wakikabiliana nazo  hasa uanzishwaji wa Mradi mkubwa wa ujenzi wa  Soko la kisasa la kitega Uchumi  Bunazi . 


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bwana John Paulo Wanga amesema kuwa lengo kubwa la Tamasha hilo ni kutafakari na kutathimini kwa kina yale yote mazuri  yaliyofanyika katika awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuuri ya Muungano wa Tanzania Doctor Samia Suruhu Hassani.

Amewahimiza watumishi wa Halmashauri hiyo kuendelea kushirikiana katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri hiyo ili kuweza kutatua changamoto wanazokabiliana nazo wananchi huku akiwahimiza kuhakikisha wanashiriki kikamilifu katika Uchaguzi mkuu utakaofanyika October .

MWISHO.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI