Header Ads Widget

CHINA YATOA MOTISHA YA $1,500 KWA WAZAZI ILI KUONGEZA WATOTO

Wazazi nchini China wanapewa yuan 3,600 (£375; $500) kwa mwaka kwa kila mtoto wao aliye chini ya umri wa miaka mitatu katika ruzuku ya kwanza ya serikali nchini kote inayolenga kuongeza viwango vya uzazi.

Kiwango cha uzazi nchini humo kimekuwa kikishuka, hata baada ya Chama tawala cha Kikomunisti kukomesha sera yake tata ya mtoto mmoja karibu miaka kumi iliyopita.

Msaada huo utasaidia karibu familia milioni 20 kwa gharama ya kulea watoto, kulingana na vyombo vya habari vya serikali.

Mikoa kadhaa kote China imefanya majaribio ya aina fulani ya malipo ili kuhimiza watu kuwa na watoto zaidi huku taifa hilo la pili kwa uchumi mkubwa duniani likikabiliwa na mzozo wa idadi ya watu.

Mpango huo uliotangazwa Jumatatu, utawapa wazazi jumla ya hadi yuan 10,800 kwa kila mtoto.

Sera hiyo itatumika mara kwa mara kuanzia mwanzoni mwa mwaka huu, shirika la utangazaji la serikali ya Beijing CCTV lilisema.

Familia zilizo na watoto waliozaliwa kati ya 2022 na 2024 pia zinaweza kutuma maombi ya ruzuku kiasi.

Hatua hiyo inafuatia juhudi za serikali za mitaa kuongeza viwango vya uzazi nchini China.


 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI