NA NAMNYAK KIVUYO, ARUSHA
Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu kazi vijana, ajira na wenye ulemavu Ridhiwani Kikwete ameitaka mamlaka ya ununuzi wa umma (PPRA) kuwatumia wanasiasa katika kutoa elimu na kutanga fursa ya asilimia 30 za zabuni za ununuzi kwa makundi maalum ya vijana na wenye ulemavu.
Kikwete ameyasema hayo wakati akihutubia katika kongamano la 9 la mamlaka ya ununuzi wa umma linaloendelea mkoani Arusha ambapo alisema kuwa changamoto kubwa iliyopo ni mapungufu ya kimfumo ambapo taarifa hazifiki kwa wakati kwa wahusika.
Ameeleza kuwa kwa kutumia kundi la wanasiasa ambao kwao kwa kutangaza fursa hizo ni sehemu ya kuonekana katika jamii, wanavyoijali na kuitambua ambapo alishauri katika vikao vijavyo wahakikishe wanawakaribisha wakurugenzi ambao ni watendaji, wenyeviti wa halmashauri na mameya wa majiji ili waje kupata elimu ili wajue ni jinsi gani watakavyoenda kuzisimamia hizi asilimia 30
Amesema elimu zaidi inatakiwa kutolewa kwa wadau ili waweze kuzikimbilia fursa hizo ambao wanapokuwa wanatenga asilimia 30 ni mihimu kwao kuzingatia kuwa watu ambao wanatakiwa kufikiwa na fursa hizo hawana uelewa wa kutosha hivyo ni jukumu lao wao ambao ni wadau katika utekelezaji wa sheria hiyo kuhakikisha kwamba wana waelewesha na kuwaambia nini wanachotakiwa kufanya.
"Wengi wanafahamu zaidi upatikanaji wa asilimia 10 kuliko asilimia 30 hizi za manunuzi ya umma kwa hiyo ninasisitiza juu ya umuhimu wa utoaji wa elimu, sijui mnanielewa? kwamba watu wanaotakiwa wapelekewe hizi fedha hawana taarifa nazo na ndio bahati mbaya sana iliyopo katika eneo hili lakini kama mtatumia wanasiasa, hao ni daraja lepesi sana la kuweza kuwafikia watu hao,"Ameeleza Kikwete
"Ili jambo ukimwezesha diwani yeye atakuwa spika phone zetu, ukimwezesha mbunge una hakika kabisa watu wataelewa hicho kitu kwani niwachache sana wanaofahamu kuhusu hizi asilimia 30 za manunuzi ya ndani na mtakapoondoka na maadhimio yenu moja ya eneo kubwa ambalo mnatakiwa muondoke nalo na kuufanya kuwampango kazi wa utekelezaji wa majukumu yenu katika mwaka wa fedha 2025/2026 lazima eneo la kutoa elimu liwe msingi namba moja kwenda kulifanyia kazi,"Amesisitiza
Amefafanua kuwa changamoto hizo za uelewa mdogo na kwa baadhi ya wanufaika kuhusu utaratibu wa kushiriki katika zabuni ziwe msingi wa mipango ya utekelezaji katika siku zijazo na ni ahadi ya serikali kuendelea kuchukua hatua madhubuti kupitia mafunzo miongozo na ufuatiliaji wa karibu ili kuziondoa changamoto hizo.
Amesema kuwa wanapojipanga kutekeleza mipango ya kimaendeleo kibajeti katika mwaka wa fedha wa 2025/2026 serikali itaendelea kuetekeleza na kuongeza usimamizi na ufuatiliaji kwa karibu katika utekelezaji wa asilimia 30 ya zabuni kwa makundi maalum ambapo ni wazi kuwa elimu zaidi inatakiwa.
Ameeleza kuwa kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022 vijana walio katika umri wa miaka 15 hadi 35 wa Tanzania bara wanakadiriwa kufika milioni 21 sawa na asilimia 34.4 ya watanzania wote huku wenye ulemavu wakiwa ni takribani watu milioni 5,251,729 sawa na asilimia 8.9 ua watanzania wote
"Hii inatoa umuhimu wa kipekee kwa serikali kuwekeza kwa dhati kwa makundi haya kwa lengo la kukuza uchumi jumuishi ambapo kwa kutekeleza agizo la kisheria la kutenga asilimia 30 za zabuni za ununuzi wa umma kwa makampuni ya wazawa na makundi maalum, ambayo imeongeza ushiriki wa vijana na wenye ulemavu katika kuchakata zabuni ambapo katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 jumla ya vikundi 119 vilipata tuzo za zabuni zenye thamani ya shilingi bilioni 4.02 ikilinganishwa na vikundi 57 vya vijana vilivyopata tuzo katika mwaka 2024/2025," Ameeleza
"Zabuni 143 zenye thamani ya shilingi bilioni 4.2 kwa upande wa vijana zilitolewa ma kwa upande walemavu vikundi vitatu vilipewa jumlabya zabuni 17 zenye thani ya shilingi bilioni 1.01 hadi kufikia mwezi Mei 2025," Amefafanua.
0 Comments