Header Ads Widget

SAUTI YAONESHA JINSI WAONGOZA NDEGE WALIVYOPOTEZA MAWASILIANO NA MARUBANI

 

Sauti iliyotolewa hivi karibuni inaonesha wakati waongoza ndege katika mojawapo ya viwanja vya ndege vyenye shughuli nyingi zaidi mjini New York walipopoteza mawasiliano na ndege zilizokuwa chini yao na kumwacha rubani mmoja akiuliza, "Tunakaribia, unatupata?". Rubani aliita mara tano kwa muda wa sekunde 30 kabla ya muongoza ndege kujibu, sauti iliyorekodiwa na LiveATC.net inaonesha.

Nyakati za wasiwasi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Newark Liberty zilisababisha wafanyikazi wengi kwenda likizo kutokana na kiwewe, na kuchangia mamia ya safari za ndege kuchelewa.

Waziri wa Uchukuzi wa Marekani Sean Duffy alisema kuwa mawasiliano yalipotea kwa sekunde 30, na kwamba hakuna ndege iliyokuwa hatarini.

Wengine wachache wamekadiria kuwa mawasiliano yalipotea kwa hadi sekunde 90. "Hizo ni sekunde 90 za anga iliyojaa kabisa ya ndege zinazoruka bila kuwa na muongozo kwenye mojawapo ya viwanja vya ndege vilivyo na shughuli nyingi zaidi Marekani," Seneta wa New York Chuck Schumer alisema Jumanne.

Sauti iliyotolewa Jumanne na LiveATC.net iko kati ya mnara wa kudhibiti trafiki ya anga huko Philadelphia, na marubani wanaoruka katika eneo karibu na moja ya vitovu vya usafiri vya New York.

"Nakaribia, unanipata?" rubani mmoja anayewasili kutoka New Orleans anasema, bila jibu. Baada ya majaribio matano zaidi, zaidi ya sekunde thelathini, mnara unajibu: "Nakupata vyema."

Katika hatua nyingine, mnara wa udhibiti unamwambia rubani wa United Airlines: "Nitakusogeza hapa kwa sababu nimeambiwa tu kwamba mbinu hiyo ilipoteza rada zote." "Skrini tatu kati ya nne za rada zilikuwa nyeusi na hazioneshi masafa."

Rubani anasikika akijibu kwa utulivu: "Sawa, tuko tayari kusonga mbele." Tukio hilo la tarehe 28 Aprili lilichangia mamia ya safari za ndege kuchelewa kuendelea hadi Jumanne.

Waziri Duffy alisema kukatika kwa mawasiliano ni "ishara kwamba tuna mfumo dhaifu, na lazima urekebishwe". Utawala wa Shirikisho la Usafiri wa Anga pia ulikiri katika taarifa kwamba "mfumo wetu wa zamani wa udhibiti wa trafiki wa anga unaathiri nguvu kazi yetu".

Shughuli za udhibiti wa usafiri wa anga katika uwanja wa ndege huko New Jersey zimekuwa na ukosoaji wa mara kwa mara hivi karibuni.

Wiki iliyopita, United Airlines ilitangaza kuwa inaghairi safari 35 za ndege kwa siku kutoka kwenye ratiba yake ya Newark kwa sababu uwanja wa ndege "hauwezi kushughulikia idadi ya ndege ambazo zimepangwa kufanya kazi hapo".

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI