Header Ads Widget

AFRIKA KUSINI YAKOSOA MPANGO WA MAREKANI KUKUBALI WAAFRIKA WAZUNGU KAMA WAKIMBIZI

 

Wazungu Afrika Kusini wakosoa mpango wa Marekani wa kuwapokea Waafrika weupe kama wakimbizi

Afrika Kusini imeikosoa Marekani huku ripoti zikiibuka zinazosema kuwa Marekani inaweza kupokea Waafrika wenye asili ya wazungu kama wakimbizi mapema wiki ijayo.

Waraka ulioonekana na mshirika wa BBC wa Marekani CBS unaelezea uwezekano wa kuhamishwa kama "kipaumbele" kwa serikali ya Rais Donald Trump, hata hivyo muda haujathibitishwa hadharani na Ikulu ya White House.

Katika taarifa iliyochapishwa Ijumaa, wizara ya mambo ya nje ya Afrika Kusini ilielezea hatua hiyo inayodaiwa kuwa "ilichochewa kisiasa" na iliyoundwa kudhoofisha "demokrasia ya kikatiba" ya Afrika Kusini.

Mnamo Februari, Trump alielezea Waafrika kama waathiriwa wa "ubaguzi wa rangi" katika agizo kuu, na kuwapa fursa ya kuishi tena Marekani.

Mamlaka za Afrika Kusini zilisema hazitazuia kuondoka kwa wale waliochaguliwa kwa ajili ya makazi mapya, lakini walisema walikuwa wametafuta hakikisho kutoka kwa Marekani kwamba wawe wamechunguzwa na kuhakikiwa kikamilifu na wasiwe na mashtaka ya uhalifu yanayowasubiri.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa madai ya ubaguzi dhidi ya wazungu walio wachache nchini humo hayana msingi wowote, na kwamba takwimu za uhalifu hazionyeshi kwamba kuna kundi lolote lililolengwa katika vurugu za mashamba.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI