Rais wa Marekani Donald Trump ametaja shambulio la Urusi dhidi ya mji wa Sumy nchini Ukraine kuwa la kutisha, lakini hakuitaja Urusi moja kwa moja.
"Nadhani ni baya. Ninaambiwa walifanya makosa. Lakini nadhani ni baya. Nadhani vita vyote ni jambo baya," Trump aliwaambia waandishi wa habari ndani ya Air Force One akielekea Washington, kwa mujibu wa CNN, AFP na Reuters.
Alipoulizwa kufafanua alichomaanisha kuwa "kosa" la Urusi, rais wa Marekani alisema: "Walifanya makosa. Nadhani ilikuwa makosa ... Tazama, ungewauliza."
Sio Trump wala Ikulu ya White House, katika taarifa iliyotolewa awali, iliyotaja Urusi kuwa wahusika wa shambulio hilo, ingawa Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alitoa rambirambi kwa "waathiriwa wa shambulio hilo la kombora la Urusi dhidi ya Sumy," AFP inabainisha.
Shambulio la kombora katika mji wa Sumy lililotekelezwa na Urusi Jumapili asubuhi liliua watu 34, wakiwemo watoto wawili, na kujeruhi 117.
Urusi haijatoa maoni rasmi kuhusu shambulio hilo au idadi kubwa ya raia waliouawa.
Makombora ya Urusi yaliwashambulia wakaazi waliokusanyika kwa ibada ya Jumapili, shambulio baya zaidi mwaka 2025, CNN inaripoti.
0 Comments