Mshambuliaji wa Misri Mohamed Salah amesaini mkataba mpya wa miaka mbili na Liverpool.
Makubaliano yake ya zamani yalikuwa yanamalizika msimu wa joto na kumekuwa na mashaka kama angesalia the Reds kufuatia maoni yake wakati wa msimu na uvumi uliomhusisha na kuhamia Saudi Arabia.
Hata hivyo, sasa atapata fursa ya kuongeza mabao yake 243 na fursa 109 alizosaidia Liverpool kufunga magoli katika mechi 393 alizocheza.
"Kwa kweli nimefurahi sana - tuna timu imara sasa," alisema Salah.
"Kabla pia tulikuwa na timu bora. Lakini nilisaini mkataba kwa sababu nafkiria tunayo nafasi ya kushinda mataji mengine na kufurahiya mpira wangu.
Salah amefunga mabao 32 katika mashindano yote msimu huu, yakiwemo 27 kwenye Ligi Kuu ya England huku the Reds wakisaka taji la 20 la ligi kuu.
Liverpool wako nyuma kwa tofauti ya pointi 11 na Arsenal wanaoshika nafasi ya pili huku wakiwa wamesalia na mechi saba.
Salah, ambaye alijiunga na Liverpool kutoka Roma mwaka 2017, ameshinda Champions League, Premier League, FA Cup, League Cup na Fifa Club World Cup akiwa na Reds.
0 Comments