China imetangaza ushuru mpya wa 125% kwa bidhaa za Marekani.
Ushuru huu umeongezeka kutoka 84% iliyotangazwa Jumatano. Ni sawa na ushuru wa sasa wa Marekani kwa bidhaa za China.
Hili limetokana na vita vya kibiashara vinavyoendelea ambapo siku ya Jumatano, Ikulu ya Marekani ilisema imeongeza ushuru wa bidhaa za China zinazoingizwa nchini humo hadi 145%, ikiwa ongezeko la asilimia 20 kutoka ongezeko la wiki zilizopita.
China inasema 'haitajibu' ushuru wa ziada wa Marekani
Wakati huo huo, Beijing inasema haitajibu ushuru wowote zaidi uliowekwa na Marekani.
Inasema "ushuru wa juu usio wa kawaida" uliowekwa na Marekani "unakiuka kwa kiasi kikubwa sheria za biashara ya kimataifa na kiuchumi, sheria za msingi za kiuchumi na ni uonevu wa upande mmoja".
0 Comments