Header Ads Widget

'WAZAWA WEKEZENI KWENU" WAZIRI BITEKO.

 


Na Shemsa Mussa -Matukio daima Blog  Kagera


Naibu waziri Mkuu na waziri wa Nishati Mhe Dotto Biteko amewataka wazawa wa mkoa wa Kagera wanaoishi nje na ndani ya nchi kutumia fursa ya Ijuka  Omuka ili kuendele kuwekeza na kuinua uchumi wa Mkoa huo


Waziri Biteko ametoa wito huo wakati akiongea katika ufunguzi wa tamasha la ijuka omuka katika ukumbi wa KCU uliopo manispaa ya Bukoba mkoani Kagera

 


Tamasha hili la ijuka omuka limebeba neno la kihaya lenye maana ya kumbuka nyumba ambao limeandaliwa na ofisi ya mkuu wa mkoa huo pamoja na wadau wa maendeleo mkoani humo lengo likiwa ni kuwataka wazawa wa Kagera  kukumbuka nyumbani na kuwekeza ili kuinua mkoa wa Kagera kiuchumi.



Kwa upande wake Waziri wa mambo ya ndani Inocent Bashungwa alisema wataendelea kushirikiana na mkuu wa mkoa huo ili kuhakikisha wanasukuma mbele  maendeleo ya mkoa huo huku akiishukuru Serikali kuendelea kuwekeza Kagera.



Naye Mkuuu wa mkoa wa Kagera Hajat Fatma Mwassa amesema tamasha hili limezaaa matunda mbali mbali ikiwa ni kuanzisha viwanda vipya mkoani humo pamoja na mambo mengi ya kimaendelea


Kwa upande wake mkurugenzi wa kuendeleza kilimo Tanzania Daktari  John Kyaruzi alisema kuwa  mradi wa uwekezaji wa vizimba mia nne hamsini tayari  umepata muwekezaji kutoka Nchini  Marekani.


 Wakati huohuo mhadhiri wa chuo kikuu Cha sokoine Daktari Philmon Nyinondi akisema tayari taasisi ya tume ya sayansi COSTEC  wametenga  fedha Kwa ajili ya utafiti wa njia Bora ya uvunaji wa senene.


Tamasha hili la pili la uwekezaji la Mkoa wa Kagera limezinduliwa rasmi leo na litaendelea mpaka Desember 26 mpaka huu.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI