Header Ads Widget

POLISI KIGOMA YAFANYA OPERESHENI MAALUM KUDHIBITI AJALI

Kamanda wa Polisi Mkoa Kigoma Filemon Makungu akizungumza na abiria waliokuwa wakisafiri na moja ya mabasi ya abiria kutoka kituo kikuu cha mabasi mjini Kigoma alipokuwa akifanya ukaguzi kuhakikisha sheria za usalama barabarani zinafuatwa

Kamanda wa Polisi Mkoa Kigoma Filemon Makungu (kushoto)  akizungumza na madereva na makondakta wa mabasi ya abiria katika  kituo kikuu cha mabasi mjini Kigoma alipokuwa akifanya ukaguzi kuhakikisha sheria za usalama barabarani zinafuatwa

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

POLISI mkoani Kigoma imeendesha zoezi la maalum la kutoa elimu kwa vyombo vya usafiri na usafirishaji kuhusu kuzingatia kufuata sheria za usalama barabarani huku ikikamata baadhi ya vyombo hivyo ambavyo havifuati sheria.

Kamanda wa polisi mkoa Kigoma,Filemon Makungu Desemba 16  alifanya ziara ya kushtukiza katika kituo kikuu cha mabasi yaendayo nje ya mkoa na nchi Jirani ambapo alizungumza na madereva na watumishi wa magari hao kuhusu kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Akizungumza na wafanyakazi wa mabasi hayo Kamanda huyo wa polisi mkoa Kigoma aliwataka wote wanaohusika na kusimamia magari hayo wakiwemo madereva na makondakta kuzingatia sheria za usalama barabara kuhakikisha magari yanafika salama lakini pia kuzingatia sheria nyingine za usafirishaji ikiwemo magari kupaki idadi ya abiria kwa kuzingatia   uwezo wa gari na kuacha  kukiuka masharti ya  leseni zao.

Kamanda Makungu alisema kuwa wakati huu wa kuelekea likizo na sikukuu za mwisho wa mwaka kumekuwa na ongezeko kubwa la abiria jambo linalosabisha magari ya abiria kukiuka sheria na taratibu za leseni zao hivyo kusababisha ajali au usumbufu kwa abiria.

Sambamba na hilo Kamanda huyo wa polisi mkoa Kigoma aliingia kwenye magari ya abiria yaliyokuwepo kituoni hapo na kutoa tahadhari kwa abiria kuchukua hatua wanapoona sheria na taratibu za usafirishaji zinavunjwa ambapo alitoa namba yake ya siku na kuwataka abiria kuwasiliana naye wanapoona kuna makosa yanatendeka.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI