Header Ads Widget

TCCIA YAAINISHA VIKWAZO 18 VYA BIASHARA YA KUVUKA MPAKA


Wafanyabiashara za mazao na nafaka wanaofanya biashara ya kuvuka mpaka


Dk.Chaboba Mkangwa Afisa tathmini na ufuatiliaji TCCIA Kigoma akitoa repoti ya utafiti alioufanya kuhusu vikwazo vikwazo vya kikodi vinavyowakabili wafanyabiashara wa mazao wanaofanya biashara ya kuvuka mpaka

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

Chama Cha Wafanyabiashara, wenye viwanda na Kilimo (TCCIA) kimeainisha vikwazo 18 visivyo vya kikodi ambavyo vimekuwa changamoto kubwa na kuzuia kukua kwa biashara ya kuvuka mpaka kwa wafanyabiashara za mazao na nafaka nchini Kwenda katika nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki.

 

Meneja ufuatiliaji na tathmini (TCCIA) mkoa Kigoma, Dk.Chaboba Mkangwa alisema hayo akitoa taarifa ya utafiti  waliofanya kwenye  vituo vinne vya ushuru wa forodha nchini vinavyoshughulikia taratibu za  kuvuka mpaka.

 

Dk.Mkangwa   akiwasilisha ripoti  kwa wadau wanaohusika na biashara na usafirishaji wa  mazao nje ya nchi   ikiwa ni sehemu ya mradi wa Kukuza Biashara kwa wafanyabiashara wa ndani kwenda katika nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki kwa Kushughulikia Vikwazo Visivyo vya kikodi  (NTBs) kwenye Biashara za mazao na nafaka mradi unaofadhiliwa na Bodi ya mageuzi ya kijani Afrika (AGRA) na Taasisi ya Bill and Mellinda Gates ya Marekani.

 

Alisema kuwa katika utafiti huo walioufanya katika hivyo vya forodha alizitaja baadhi ya changamoto hizo kuwa ni Pamoja na malalamiko ya  tozo na kodi zinazotozwa mara mbili, wanunuzi katika nchi nyingine za Afrika Mashariki kupanga bei badala ya bei kupangwa na mwenye bidhaa , gharama za uendeshaji kuwa juu, tuhuma za rushwa na hongo na changamoto za uelewa mdogo kwa wafanyabiashara wa usafirishaji bidhaa nje na uingizaji biashara nchini

 

Sambamba na hilo alisema kuwa wafanyabiashara wengi wanakabiliwa na changamoto ya kutojua lugha kwa nchi wanazoenda kufanya biashara, rushwa na urasimu katika kupata vibali, kutokuwepo kwa masoko ya Pamoja kwenye maeneo mengi ya mipakani na masoko yasiyoaminika, serikali kuzuia baadhi ya mazao kuuzwa nje bila kuwepo taarifa rasmi kwa wafanyabiashara.

Akizungumza katika mkutano huo Katibu wa TCCIA mkoa Kigoma, Prosper Guga alisema kuwa mradi huo unalenga kuibua na kuaninisha vikwazo visivyo vya kikodi vinavyowakabili  wanawake na vijana wanaofanya biashara ya  mazao Kwenda nje ya nchi ili kukabiliana na vikwazo hivyo kuwezesha kuongeza ukubwa wa biashara ya kuvuka mpaka inayofanywa na wanawake na vijana.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI