Header Ads Widget

WADAU WA HAKI JINAI WATEMBELEA SHUGHULI ZA BANDARI KIGOMA

 
                         
Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Augustine Rwizile   (watatu kushoto) akiongoza wadau wa Haki  jinai mkoa Kigoma kutembelea shughuli za mamlaka ya bandari (TPA) katika bandari ya Kigoma ili kuona shughuli za bandari hiyo kuweza kuwasiaidia katika kuendesha mashauri yao mahakamani - (Picha na Fadhili Abdallah)
Stanislaus Kagisa Mkurugenzi wa sheria Mamlaka ya bandari (TPA) akitoa maelezo ya utendaji wa bandari kwa wajumbe wa Haki jinai mkoa Kigoma.
Wadau wa haki jinai na wadau wa bandari wakifuatilia taarifa ya utendaji wa mamlaka ya bandari kuhusu bandari za ziwa Tanganyika kutoka kwa uongozi wa TPA.

Na Fadhili Abdallah, Kigoma

Wadau wa haki jinai mkoa Kigoma wamefanya ziara kutembelea shughuli za mamlaka ya bandari katika bandari ya Kigoma na Kibirizi mjini Kigoma  ili kuwezesha kuwa na uelewa mpana wa shughuli za bandari iweze kuwasaidia yanapotokea mashauri mahakamani kuhusiana na jambo lolote la kesi za jinai na madai zinazotokea bandarini.

 Mkurugenzi wa huduma za sheria wa Mamlaka ya bandari nchini (TPA), Stanslaus Kagisa akizungumza wakati wa  warsha ya siku mbili kwa wajumbe wa kamati ya Haki jinai mkoa Kigoma alisema kuwa TPA imelifanya jambo hilo kuwapa uelewa na kujua kwa undani shughuli zinazofanywa na taasisi hiyo ili shughuli za mashauri ya kisheria zinazohusu mamlaka hiyo ziweze kushughulikiwa kwa haraka na kwa uelewa mpana.

 Kagisa alisema kuwa serikali inafanya uwekezaji mkubwa katika bandari zake ikiwemo bandari za ziwa Tanganyika ikiwemo za mkoa Kigoma hivyo mabilioni hayo yanaongeza hatari yakuongezeka kwa mashauri ya jinai hivyo Majaji,Mahakimu, wapelelezi, ofisi ya Mwendesha mashitaka wanapojua kwa undani shughuli za bandari watasaidia kuharakisha kesi lakini maamuzi yao kuzingatia sheria na hasara inayoweza kupatakana katika uwekezaji huo.

                               
Akizungumza katika warsha hiyo baada ya kupata maelezo ya uendeshaji wa bandari na kutembelea bandari za mkoa Kigoma Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Augustine Rwizile alisema kuwa mwenendo wa kesi wanazosimamia na hukumu wanazotoa zinazingatia sheria lakini kuwa na uelewa mkubwa wa eneo ambalo kesi inazungumziwa inatoa picha ya hukumu inayostahili kutolewa.

 

Alisema kuwa ziara waliyofanya katika bandari za mkoa Kigoma inawapa picha ya namna gani wasimamie kesi hizo kwa uharaka wake na kwa maslahi ya Taifa hasa kwa miradi ya kimkakati kama hii ya bandari hivyo ziara hiyo kwao imekuwa na manufaa makubwa katika kurahisisha utendaji kazi wao.

 

Kwa upande wake Mkuu wa  Upelelezi na makosa ya jinai mkoa Kigoma, Alfred Kasolo alisema kuwa bandari ni eneo la kiuchumi na biashara ambalo linatoa fursa ya upatikanaji wa pesa hivyo kuwepo kwa makosa mengi ya jinai na madai hivyo wao kama wadau wa haki jinai mafunzo na ziara hiyo itakuwa na tija kubwa katika utekelezaji wa majukumu yao ya upelelezi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI