Header Ads Widget

TASAF IMERUDISHA TABASAMU LA FAMILIA YANGU BAADA YA KUTELEKEZWA NA MUME WANGU

           Na  Matukio Daima Media App,

KISA Lauden mkazi wa Ghana Jijini Mbeya mama wa watoto watano amesema kuwa baada  ya kuingizwa kwenye mfuko wa maendeleo ya Jamii (TASAF )maisha yake yamebadilika kwa familia yake  kula  milo miwili baada ya mlo mmoja wa awali  kwa siku  huku wakilala kwenye mkeka.


Bi.Lauden amesema kwamba changamoto za kimaisha alianza kuzipata baada ya mume wake kumtelekeza  baada ya kukataa kutoa mimba  yake ya tano na hivyo kumuacha  akiteseka na  watoto  na kutokomea kusikojulikana tangu mwaka 2006 mpaka sasa.


Akizungumza na Matukio Daima Media October 24,2024 jinsi TASAF ilivyoweza kumwinua kimaisha na familia yake ,Kisa Lauden amesema kuwa baada ya Kuonwa  na mfuko huo  maisha yake  imekuwa miujiza kwani yamekuwa na mabadiliko .


"Hali yangu ya kimaisha niliyokuwa nayo kipindi hicho ilikuwa ni ngumu kulisha watoto ilikuwa ni ngumu  watoto  kupata chakula pamoja kusomesha  yaan ilikuwa  changamoto wakila.mlo mmoja  ambayo ni mchana basi mpaka kesho  yake,mume wangu tuliachana mwaka  2006 kwa hiyo kusomesha watoto juu yangu kula  watoto ,mavazi vyote ilikuwa kupitia TASAF  na nilipoingizwa kwenye mfumo huu nilishukuru nimeona matunda yake kwani serikali imekuwa msaada mkubwa"amesema.


Akielezea zaidi amesema kuwa viongozi wa TASAF walishauri kutengeneza vikundi na kusema fedha wanayopewa wasile yote bali wanunue mahitaji ya watoto , kununua chakula na kufanya biashara ambayo itakuwa mkombozi kwao katika kujiinua kiuchumi.


Meleckzedeck Nduye Ofisa Habari wa mfuko wa maendeleo ya Jamii (TASAF) amesema kuwa  moja ya marshati ambayo wanawapa wanufaika wa mfuko huo  ni kuhakikisha fedha hizo zinawanuisha kama kaya ili waweze kuinua uchumi wao  na kuondokana na dibwi la umasikini uliokithiri ambao  waliwakuta nao.


"Sasa hivi tunazungumza zaidi ya miaka  miaka nane ( 8 )toka  tumeanza uhamilishaji  wa fedha hizi kwa walengwa  na tumeona matokeo makubwa walengwa wetu  wengi walikuwa na hali mbaya lakini sasa wanaweza kusimama wenyewe kwa miguu yako na wanapata milo mitatu wanaweza kuja kwenye matukio makubwa ya kitaifa  kama haya na kuonyesha vitu ambavyo wanafanya katika hali halisi isingekuwa kawaida lakini kazi ni njema kwani walengwa wanafanya vitu vinavyoonekana ambavyo vinatokana na kazi ya mikono yenu"amesema Ofisa Habari huyo.


Aidha Nduye amesema kuwa siri ya mafinikio kwa walengwa ni TASAF  kuwapa  elimu ya umoja ,kujiunga kwenye vikundi,elimu ya kuweka na kukopa ambayo inasaidia kukua kwa haraka na kufanya vitu vikubwa kwa wakati mmoja.


Mfuko wa maendeleo ya Jamii (TASAF)upo kwenye maadhimisho ya huduma za fedha kitaifa ambayo yalianza October 21,2024 na yatahitimishwa October 26 mwaka huu.


 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI