"Kumradhi Waziri Lukuvi"
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), William Lukuvi, analengwa kuchafuliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Katika toleo lake la 26 Septemba mwaka huu, gazeti la MwanaHALISI liliripoti katika ukurasa wa mbele, kuwa Lukuvi anataka Rais Samia abakie madarakani hadi mwaka 2035, lakini mwenyewe amekana kutamka maneno hayo.
MwanaHALISI Online limeona video inayomuonyesha Lukuvi akizungumzia jambo hilo, lakini baada ya uchunguzi wake imeonyesha kuna kila dalili kuwa imehaririwa kwa nia mbaya.
Baada ya majadiliano ya kina na kiongozi huyo, tumekubaliana kwa kuchapisha maudhui hayo, tumemkosea na kwa sababu hiyo tunamuomba radhi.
Mhariri.
0 Comments