Header Ads Widget

MTOTO ALIYEMUUA BABA YAKE, AACHIWA HURU GEITA


Na matukio daima App,


Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Geita imemuachia huru Mahele Petro (19), mkazi wa Nyamilembe wilayani Chato mkoani Geita baada ya kukiri kosa la kumuua baba yake kwa kumchoma mkuki shingoni bila kukusudia.


Hukumu imetolewa leo Septemba 24, 2024 na Jaji Athuman Matuma, aliyesema Mahakama inamuachia huru mshtakiwa kwa sharti la kutotenda kosa la jinai kwa miezi 12.


Akisoma hukumu, Jaji amesema mshtakiwa alimuua baba yake mzazi, Petro Lyamba mkazi wa Kalebezo kwa kumpiga kwa mkuki shingoni kutokana na hasira zilizosababishwa na mgogoro wa kifamilia.

Amesema kutokana na hoja zilizojengwa na wakili wa mshtakiwa, Erick Lutehanga kama shufwaa kwa ajili ya nafuu ya adhabu imetiliwa maanani. Pia, kosa hilo ni la kwanza kutendwa na mshtakiwa kama upande wa mashtaka ulivyoeleza.

“Kwa mazingira hayo mshtakiwa anastahili nafuu ya adhabu. Hata hivyo, tayari amekwishatumikia adhabu kimsingi kwa kukaa rumande kwa miaka mitatu na miezi saba. Maisha yake hayawezi kuwa mazuri kwa kiasi ambacho yangekuwa kama asingetenda kosa hili,” amesema.

“Amemuua baba yake hata kumrudisha nyumbani si jambo jepesi kwake, kwa sababu anahitajika bado kutengeneza maisha yake na familia yake kutengeneza mahusiano yaliyopotea kutokana na tukio hili,” amesema Jaji Matuma.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI