Header Ads Widget

MATAMSHI YA DKT NCHINBI NA UKOMAVU WA KISIASA


  MWANDISHI WETU, - MATUKIO  DAIMA APP

Matukiodaima3@gmail.com


MATAMSHI  yaliotamkwa  hivi karibuni  na Katibu  Mkuu wa  Chama Cha Mapinduzi (CCM  )BALOZI Dk  Emmanuel  Nchimbi katika mkutano wake na Wahariri wa Vyombo  vya habari  yamesaidia mno shusha joto na  upepo wa taharuki ya kisiasa nchini.


Amejitahidi kadri ya uwezo wake  kulileta taifa pamoja dhidi ya tisho la mgawanyiko unaopigiwa chapuo  baadhi ya watanzania walioko nje ya nchi.


Kwa wiki  kadhaa  sasa kumekuwa na piga nikupige ya kuturushiana  maneno makali katika jamii kwa maneno yenye jazba yakikosa ukweli  matiki ya kujenga umoja wa Kitaifa.



Mfululizo wa  kuripotiwa watu  kutekwa na kwenda kusikojulikana  ,kumezidisha i wasiwasi na hofu  ikiwemo  tukio  la kuuawa kwa Mjumbe wa sekreteriet  ya CHADEMA marehemu Ali Mohamed  Kibao .


Kifo cha Kibao kilikaribia kuzidisha chuki na  hamaki lakini pia  kuibuka kwa mabishano yaliokuwa na  mitazamo hasi baada ya kutanda  huzuni, mlajonzi na hofu. 



Kwa watu waliomsikiza kwa umakini Dk Nchimbi, wamemsikia alioyanena  Ametamka maneno mazima yatokanayo na ukweli  wa historia ya nchi yetu tokea kuzaliwa kwa jamhuri ya muungano  wa Tanzania mwaka 1964


Yalikuwa ni matamshi yenye mpangilio na sentensi zenye  mashiko. Hotuba yake ya saa kadhaa ,yamebeba ukweli na uhalisia wa mambo  jinsi yanavyotakiwa yawe muda wote   .


Amekutana waandishi wa habari katika wakati  muafaka.Ameitendea haki hadhira  aliokutana nayo ,na  kupitia mkutano  wake  huo  dhamira ya Dk Nchimbi imeeleweka na kila mtu aliyemsikia.


Kutokana na maelezo yake amejiandaa kabla  hajitokeza kwa muda sahihi .Dk Nchimbi hakukurupuka  ila yaonyeaha amesema anakwenda  kusema Taifa limsikie.Kwa hakika kabla ametafakari kisha  akasema .


Hakutaka kabisa kusema ili  ionekane amesema, badala yake amepania kusema anayoyaamini na kuweza kuyatetea  kwa nguvu ya hoja .


Amekuja mbele ya  Taifa  ilhali akiwa na  maneno kamili ya  kusema na hakika  amesikika . Hivyo  watanzania nao hawanabudi kumsikiza aliyoyasema na kuyazingatia.


Katibu  mkuu huyo  wa ccm kwa kiasi kikubwa amefanikiwa kushusha joto  zito  lililotandaa kwenye  Taifa  kufuatia matukio ya kutisha. .


Amesafisha upepo  yabisi na kulirudisha taifa juu ya mstari.


Ametumia maneno mazuri na kutoa  mifano hai ,misamiati adimu lakini  yenye ukweli utokanao na  mapitio ya  historia ya Taifa letu. 



Ameizungumza kwa ufupi  lakini kwa undani wa historia ya  usalama wa nchi yetu


.Ametaja misukosuko migumu   iliolikumbana taifa lakini kwa bahati tukavuka pamoja .


Licha ya  nchi yetu  kupitia  dhoruba kali lakini tumerudi  tukiwa pamoja.Tumebaki na umoja  weru kwa miaka yote sitini ya kujitawala kwetu. 



Vilevile Katibu  huyo mkuu  ameonyesha  juhudi ,bidii na  kazi ngumu ya  jeshi la polisi  miaka kwa miaka likisimamia uliizi wa nchi  na usalama wa raia na mali zao.


Ni kweli  kuna  baadhi ya nyakati  mambo huendeshwa kisengere nyuma   katika baadhi ya  wakati .Mambo mengine tunajua  hufanyawa na baadhi tu ya askari   wazembe wasioheshimu misingi ,maadili, taratibu na  nidhamu  ya jeshi hilo .


Kwa sehemu  kubwa askari wa aina hiyo ndiyo wanaolipaka  nuksi na mikosi jeshi la polisi kwa kwenda kinyume na  mafunzo, mfumo ,kanuni ,taratibu na heshima ya polisi.


Kazi za polisi  si za  kimzahamzaha. Kila polisi hutakiwa kufuata taratibu zilizowekwa ilkutimiza haki na  wajibu wa kutumikia watu wananchi na  marufuku kufanya  maonevu au kubambikia watu kesi .


Kazi za polisi ni ngumu lakini  pia ni nyepesi  ikiwa polisi  mhusila atatimiza kazi  zake lwa mujibu sheria  na utii wa katiba ya nchi.Polisi ndio  wenye haki ya  kuwalinda raia.


Polisi hutakiwa kujua na kuhakikisha usalama raia ,   mali zao na Taifa zima  usiku na mchana  tokea tulipojitawala zipo mikononi mwao



Si kwamba  Dk Nchimbi ameeleza kwa hisia   kali bali  pia ametumia lugha  ya kiungwana na  kidiplomasia  iliokuwa  fasaha na kueleweka .Kisaikoljia na kifikra ameonyesha kukerwa na matukio  yanayotajwa  kutokea.


Amelikumbusha Taifa  kwa kuonyesha  maarifa ,ukomavu na upeo  alionao kisiasa na kionngozi  ikiwemo kutumia hekima  na busata alizojaaliwa .


Kujitokeza kwake  mbele ya Wahariri hakwenda kwa kutumia mkongojo au  kutetea  sera za chama  chake  ,ameulizwa maswali mazito na kujibu kwa uwazi na  kujiamini.


Amejibu kwa mintarafu ya kujenga taifa, kuziba nyufa na kujenga ukuta.


 Kwani kiongozi huyo amezumgumza ukweli  mtupu  akioyesha jinsi asivyoridhika kwa  mambo yaliotokea  . 


Amekumbusha  haki  na wajibu kwa  kila moja kua dhamana alionayo na  kulinda thamani ya utu, ubinadamu wa kila mmoja .


Ametaka haki za binadamu zilimdwe   na kuheshimu  utawala wa sheria. 


Aidha hotuba ya Dk  Nchimbi pamoja  na maswali  alioulizwa kujibu , hayawezi kutiliwa shaka aidha na viongozi  wenzake wa kisiasa, dini, mashrika hiari ya kijamii ,jumuiya  za  kimataifa na  wanadiplomasia kwa kile alichokieleza.


Maelezo  yake yana ufafanuzi aliotokana na taharuki iliokuwepo katika  kichaka cha hofu , ni maneno yaliohitimisha utata wa sakata  zima huku akiliachia kazi  jeshi la polisi lijipange .


Wapo waliotazamia pengine wanasiasa wenzake wa vyama vingine nao  wakitokeza ili kuyauga mkono matamshi hayo  bila kujali itikadi  za kisiasa na mitazamo ya vyama vyao. 


Ikiwa tulijenga Taifa  pamoja huku tukikomboa mataifa  mengine, tukakabili majanga ya  ukame, vimbunga ,mvua,jau, mafuriko hadi kufikia kula  mahindi ya njano  ,hatimaye tulivuka salama  ,hivyo hakuna gumu linalotushinda jama tutaendelea kulinda misingi ya amani na umoja wa Kitaifa.


Tumepambana kwa gharama kubwa kupinga  ubaguzi wa rangi  kusini mwa Afrika;tulipaza sauti  kukemea ukandamizaji haki, mauaji huko Mashariki  ya Kati  na kila pembe ya dunia .


Tutukipigania  pqmoja haki za binadamu wenzetu na kusimama kwenye vyombo vya kimataita  tukisema kama Taifa ,hivyo basi katu watanzania  tusikubali kugawanywa na kugawanyika.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI