Header Ads Widget

KUTUMIA MAJIBU YA MKEMIA MKUU KUELEZA WANANCHI KWAMBA DAWA FULANI INATIBU SIO SAHIHI - NAUJA

 



 Na Thobias Mwanakatwe, SINGIDA 

OFISI ya Mkemia Mkuu wa Serikali imeeleza kuwa si sahihi Kwa  wadau ambao wamekuwa wakitumia majibu ya uchunguzi  yanayotolewa na ofisi hiyo kwa kuwaeleza  wananchi kwamba dawa fulani inatibu ugonjwa  kwa lengo la  kuvutia wateja.

Hayo yamemwa na Mkemia Mwandamizi wa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali, Ramadhani Nauja  katika mahojiano kwenye maonesho ya Mifuko na Programu za Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi yanayofanyika mjini Singida.

Alisema kitu anachokifanya Mkemia Mkuu wa Serikali si kuthibitisha kwamba dawa hii inatibu ugonjwa fulani bali ni kuhakikisha ubora wa dawa hiyo kwamba haina madhara kwa mtumiaji.

"Kuthibitisha kwamba hiyo dawa inatibu kweli au laa hilo sio jukumu la Mkemia Mkuu wa Serikali, bali jukumu la mamlaka ni kuangalia ubora wa bidhaa husika kwa afya ya watumiaji," alisema.


Aidha, aliwashauri   wadau hao  kuacha kutumia majibu ya uchunguzi unaofanywa na Mkemia Mkuu wa Serikali kuieleza jamii kuwa dawa hiyo  imethibitishwa na Mkemia Mkuu wa Serikali kuweza  kutibu

Aliongeza kuwa serikali imefanya uwekezaji mkubwa  kwenye mitambo ya kisasa ili kwenda na kasi ya teknolojia na kuharakisha  utoaji wa haki nchini.

"Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali  imepata ithibati ya ubora  wa kimataifa hivyo matokeo ya uchunguzi  katika Maabara hii yanatambulika kimataifa," alisema.


Kuhusu maabara ya uchunguzi wa vinasaba vya binadamu, alisema m  huduma hiyo imekuwa ikisaidia jamii katika  uchunguzi wa kujua  uhalali wa wazazi kwa mtoto,  kutatua changamoto ya kujua mahusiano ya kindugu katika  masuala ya mirathi. 

Alisema pia DNA imekuwa ikisaidia katika  masuala ya kitabibu mfano wanaotaka kupandikizwa figo au uroto lazima wote hao waweze kupima na kujua mahusiano ili viungo vinavyopandikizwa katika miili yao visilete madhara kwa yule anayewekewa.

"Maabara ya vinasaba vya binadamu inatusaidia kubaini masuala ya jinai kwa watu wanaoshiriki matukio ya uharifu,wizi,unyang'anyi,ujambazi ,hawa wote huwa tunawafanyia uchunguzi," alisema.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI