Header Ads Widget

CDF MKUNDA AWALETA WANEDHARLAND KUWANOA MAKOCHA WA MPIRA TIMU ZA MAJESHI

 


 Na Matukio Daima Media, Dar es Salaam 


MKUU wa Majeshi ya Ulinzi (CDF),Jenerali John  Mkunda kupitia uratibu wa baraza la michezo la majeshi ya ulinzi Dunia( conseil International du sports Military) imewaleta wakufunzi na wataalum kutoa mafunzo ya makocha,  lengo ni  kuwaaendeleza maofisa na askari wenye taaluma ya  ukocha wa mpira wa miguu kuunga mahusiano  mazuri yaliyofanywa kati ya Tanzania na  Nedharland.



Aidha dhamira ya CDF ni kupata walimu wazuri watakao saidia timu za Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) zinazoshiriki ligi mbalimbali nchini na za Taifa.



Wakizungumza kwa nyakati tofauti makocha ambao ni maofsa wa JWTZ na askari wamemshukuru CDF kwa kuona umuhimu wa mafunzo hayo kwa makocha na kwamba  wakufunzi wa TFF wamekuwa wakitoa mafunzo mbalimbali lakini walimu hapo  wakigeni wana ujuzi zaidi na vifaa  hivyo wanatoa ahadi ya kufanya vizuri katika kuhakikisha timu za majeshi na Taifa zinafanya vizuri.



Mafunzo  haya ni ya wiki mbili na ijumaa jioni yatafungwa rasmi hii inatokana na mahusiano mazuri ya Chama Cha Mpira wa miguu Cha majeshi .

Mwisho

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI