Header Ads Widget

MNEC ASAS AGEUKA MBOGO ATAKA BARABARA YA MCHEPUKO IRINGA MJINI IKAMILIKI HARAKA

MJUMBE  wa  Halmashauri  kuu ya  chama  cha mapinduzi Taifa (NEC) Salim Abri Asas amefanya  ukaguzi wa  ujenzi  wa  barabara  ya  mchepuko ya  mji  wa  Iringa kati ya  Igumbilo -Tumain na  kuagiza  ujenzi  wa  barabara   hiyo ambao  umesimama kwa  muda  mrefu  kukamilishwa  kwa   wakati  ili  kusaidia  kupunguza msongamano wa  magari  katikati ya mji wa Iringa .


MNEC  Asas  alisema awali maombi ya wananchi  wa mji  wa  Iringa na viongozi  ilikuwa  ni  kuiomba serikali  kuwezesha   ujenzi wa  barabara  hiyo ila   serikali sikivu ya  chama  cha mapinduzi chini ya  Rais wa awamu ya  sita  Dkt  Samia  Suluhu Hassan ilisikia ombi hilo la  wananchi  wa Iringa na  kutenga fedha  zaidi ya  shilingi bilioni 41  kwa  ajili  ya  ujenzi  wa barabara  hiyo na tayari  mkandarasi  wa  kujenga  barabara   hiyo amekwisha patikana hivyo kwa  sasa  CCM inatamani  kuona  ujenzi  huo unakamilika haraka.





Kwani  alisema  kuwa  iwapo  barabara  hiyo  itakamilika kwa wakati  itakuwa na faida  kubwa kwa   wananchi  wa mji  wa Iringa  pia  kwa  mikoa ya nyanda  za juu kusini  ambao  wanatumia barabara  hiyo  kuelekea  mikoa ya kanda ya nyanda  za  juu kusini na nchini za  kusini mwa Afrika ambao  wanatumia barabara   hiyo  kupitia Dodoma ,Arusha  na  nchi kama za  Kenya  na Uganda .


" Serikali yetu  ya awamu ya  sita  chini ya  Rais  wetu  mpendwa  Dkt Samia Suluhu Hassan tayari  imetenga  fedha  kwa  ajili ya ujezi  wa  barabara  hii ambayo ni barabara muhimu  sana kwetu  wana Iringa hivyo  niwaombe  wale  ambao wamepewa  kazi ya ujenzi  wa  barabara  hii  kufanya kazi  hii kwa uadilifu mkubwa na haraka  zaidi  ili  iweze  kusaidia  wananchi  " alisema .MNEC  Asas


Hata  hivyo  akizungumza na  wajumbe  wa Halmashauri  kuu ya  CCM wilaya ya  Iringa  mjini MNEC  Asas  alisema  kuwa  chama  hicho   kitaendelea  kushinda  chaguzi  za  serikali  za  mitaa na  uchaguzi  mkuu mwakani iwapo  wana CCM wataungana na kuwa  kitu  kimoja  na  wenye  kukitazama  chama   na sio  kujitazama  wao  wenyewe  kwani  chama  hicho  ni kikubwa  kuliko  mtu mwana chama  yeyote  .


Hivyo  aliwataka   viongozi  wa CCM waliochaguliwa na wananchi  kutotembe  mabega  juu  wakitaka wanachama   kuwaheshimu  wao  pasipo kufanya kazi  ila wanapaswa  kujinyenyekeza  kwa wanachama na kutekeleza majukumu yao na ilani ya uchaguzi kwa  kuzingatia  misingi ya chama  hicho .


MNEC Asas  alisema  kuwa  chama  chochote  cha  siasa ni  kutawala hivyo  ni lazima kila  kiongozi  wa  CCM kuhakikisha anawajibika na kutimiza malengo ya  chama   hicho  kwa  kutekeleza  vyema  ilani ya  uchaguzi  kwa  kuwatumikia  ipasavyo  wananchi na si vinginevyo .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI