Header Ads Widget

MJUMBE WA TAIFA WA NaCoNGO MKOA WA IRINGA AOMBA USHIRIKIANO,AIANGUKIA OFISI YA RC IRINGA KUWAPA OFISI

 


Mjumbe wa Taifa   wa  baraza la  mashirika  yasiyo  kuwa ya  kiserikali (NaCoNgo)  mkoa  wa  Iringa  Fidelis  Filipatali  amewataka   wajumbe  wa  baraza  hilo  kufanya kazi  kiwa  udshirikiano  ili  kuwezesha   ufanisi   ili  kuwezesha  NaConGo  kutambulika  zaidi kwa  jamii.

Akizungumza  leo  wakati wa  mkutano  wa kwanza  wa NACONGO  uliofanyika  ukumbi  wa  Iringa  Sun Set  Hotel mwenyekiti  huyo  alisema  kuwa  kuwa  lengo la  serikali  kuunda baraza  hilo  ni kutaka mashirika  kufanya kazi  zao  pasipo  kuingiliwa na  serikali  kwa lengo la  uratibu na kuwa na kusimamia shughuli zao wenyewe.

Hivyo alisema kupitia Baraza hilo wajumbe Wanapaswa kufanya kazi kama timu Moja ili kuwezesha Baraza hilo kuwa na mafanikio makubwa na kuwa tofauti na maeneo mengine .


Alisema  kuwa   pamoja na  NACONGO   kujulikana  kitaifa  ila  huku  chini  bado  haijajulikana  vilivyo   hivyo  kwa  upande wa  mkoa wa Iringa  wamejipanga  kuitambulisha  vema  kwa  jamii ili  kila mmoja  afahamu majukumu ya  NACONGO  na  kazi  hiyo  inahitaji  ushirikiano kwa  wajumbe  na  viongozi  wote .

Filipatali  alisema  kuwa  NACONGO  mkoa  wa  Iringa  imekusudia  kuendelea  kufanya kazi na  serikali ili kwa pamoja  kufanikisha  kutoa  huduma bora  kwa  umma.

Hata  hivyo  mwenyekiti  huyo mpya wa NACONGO  mkoa wa Iringa ambae  amepokea  kijiti  kutoka kwa  mtangulizi  wake  John Kiteve alisema  ataendelea  kufanya kazi kwa kushirikisha  wajumbe na vikao  na mikutano  itakuwa  sehemu ya  utendaji  wake kazi .

Katika hatua  nyingine  Filipatali  alisoma  barua  ya utambulisho  kutoka  Taifa  ambayo  inamtambulisha  Rasmi  ngazi ya  mkoa   huku  akiomba  kwa  upande wa  mkoa  kushusha  utambulisho  wa viongozi  wa NACONGO ngazi za  Halmashauri  ili  pia  watambulike.

Awali  mtangulizi  wake  kwa nafasi ya  uenyekiti  John  Kiteve  alimpongeza  mwenyekiti  huyo  mpya kwa  maono yake na jinsi  alivyoanza kazi kwa  vitendo na  kuwa kwa  upande wake  toka  amekuwa  mwenyekiti wa NACONGO mkoa wa Iringa  hajawahi  kuitisha  mkutano kama   huo  zaidi ya kukutana  mitaani .


Wajumbe  wa  mkutano  huo  wakiongozwa na Lediana Mafulu Mng'ong'o waliomba  ofisi ya  msajili wa mashirika  yasiyo ya  kiserikali mkoa wa Iringa   kusaidia  kupatikana kwa  ofisi ya  NACONGO  mkoa wa Iringa  ndani ya  ofisi ya mkuu wa mkoa wa Iringa  ili  kuwezesha  kufanya kazi kwa pamoja  huku  akimshukuru  Rais  Samia Suluhu Hassan  kwa  kuendelea   kuyatambua  mashirikana  hayo.

Msajili  wa mashirika  yasiyo ya  kiserikali  mkoa  wa Iringa Saida Mgeni  alisema  kuwa  mkoa  wa Iringa una mashirika  yasiyo ya  kiserikali  zaidi ya 400 ila  upatikanaji  wa mashirika hayo  huwa mgumu  sana  pale yanapohitajika  kutoa taarifa   zao  hivyo  kupitia NACONGO itakuwa rahisi  zaidi  kuyapata  iwapo  watapata  ofisi  ndani ya  ofisi ya  mkuu wa  mkoa wa Iringa .

Alisema kwa mwaka Jana alipata changamoto ya Baraza hilo la NACONGO kutokutana kwa zaidi ya Miaka miwili hivyo anategemea Kwa sasa haitatokea tena.



Mwenyekiti wa NACONGO na wajumbe wake

Mjumbe Jane Mwalembe 

Mjumbe mstaafu wa NACONGO Mkoa wa Iringa John Kiteve akitoa neno 




Mjumbe wa Baraza la NACONGO Mkoa wa Iringa Lediana Mafulu akimpongeza Msajili wa NGOs mkoa wa Iringa 
Mwenyekiti wa NACONGO Mkoa wa Iringa Fidelis Filipatali katikati akiwa na wajumbe wa Baraza hilo na Msajili wa NGOs mkoa wa Iringa Saida Mgeni wa pili kushoto 

Mkurugenzi wa Iringa Sunset Hotel akimpongeza mjumbe wa Taifa wa NACONGO Mkoa wa Iringa Fidelis Filipatali  (kulia)






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI