Header Ads Widget

BREAKING:MOTO WATEKETEZA VIBANDA VYA MACHINGA MSAMVU

 


MOTO mkubwa umeibuka kwenye vibanda  vya wafanyabiashara wadogo waliojenga kando ya kituo cha mabasi cha Msamvu  ambapo vibanda zaidi ya kumi Kati ya 60 vilivyo eneo hilo vimeteketea.


Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wamesema hili sio tukio la kwanza kutokea katika eneo hilo na inasadikiwa chanzo ni jiko la mkaa.


Hata hivyo Afisa Operesheni  wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Morogoro, Mrakibu Msaidizi Daniel Myalla amesema bado waaendelea na uchunguzi kubaini chanzo cha moto huo ingawa katika hatua za awali wamefanikiwa kuudhibiti ili usilete madhara zaidi.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI