Header Ads Widget

VYAMA 11 VYA SIASA VYALAANI KAULI ZA TUNDU LISU

 


NA MWANDISHI WETU, ZANZIBAR 

KUFUATIA Kauli za hivi karibuni za Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA -Tundu Lisu, Vyama 11 vya Siasa Zanzibar vimelaani vikali kauli hizo ambazo wanadai kuwa ni kauli za Kebehi na uchochezi zinazolenga kuleta ubaguzi kwa Watanzania kupitia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Akitoa wasilisho la Pamoja la Viongozi wa Vyama 11 vya Siasa juu ya kauli hizo, Mwenyekiti wa Chama cha ADA TADEA Juma Ali Khatib amesema kauli zilizotolewa na Tundu Lissu ni kauli za kibaguzi ambapo wameziomba mamlaka husika ikiwemo Msajili wa vyma vya siasa pamoja na vyombo vyengine kuangalia kwa makini hatua za kiongozi huyo na chama chake na kuchukua hatua zinazostahiki.

"Sisi Vyama 11 vya siasa hatuungi mkono kauli zako Tundu lisu na tunazilaani, matamshi yako ya kibaguzi kwa kuonesha wazi wazi watu wa upande mmoja wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hawana haki ya kufanya kazi upande mwingine na huu ni ubaguzi, uchochezi na kuonesha wazi wazi umefilisika kimawazo, kifikra na kisiasa na kutafuta Kiki za kisiasa,"amesema.

"Kwa msingi huu alioonesha Makamo Mwenyekiti wa CHADEMA ni dhahiri anawaambia wananchi kwamba yeye ni mbinafsi, mwenye uchu wa madaraka, mchonganishi, mfitinishaji na mwenye dhamira ovu kwa Muungano wetu," ameongeza.

"Tunavitaka vyombo vya ulinzi na usalama nchini, pamoja na msajili wa vyama vya siasa kufanya uchunguzi wa kina juu kauli anazozitoa ndugu Tundu Lissu kupitia kwenye majukwaa ya kisiasa kama ni za kwake au anatumwa na chama chake na ikithibitika Msajili wa vyama kisiasa achukuwe hatua kwa mujibu wa sheria kutokana kuwa kauli hizo zinalengo la kuligawa taifa letu," ameeleza

"Vyombo vya ulinzi na usalama na wao wachukue hatua stahiki dhidi yake au chama chake ili iwe somewhat tabia hii," amefafanua.

Amesema kuwa, ni ukweli usiopingika chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan Taifa la Tanzania limezidi kuimarisha kwa kuwepo umoja na mshikamano zinatokana na juhudi zake za kuimarisha demokrasia nchini

Aidha Mwenyekiti huyo amesitiza kuwa, kuruhusiwa kwa mikutano ya hadhara na shughuli za kisiasa kusiwafanye viongozi wa siasa kuvuka mipaka na kuwatukana viongozi hadharani pamoja na kutoa kauli za uchohezi na ubaguzi ambazo zinaweza kuhatarisha usalama wa nchi.

"Ni ukweli kuwa Dkt. Samia amefungua mikutano ya hadhara ili viongozi wa vyama vya siasa wanadi Sera zao kwa wananchi na si kutumia vibaya ruhusa hiyo," ameeleza.

Kwa upande wake Mwanaharakati wa Haki za Binadamu Ali Makame Issa amewataka Watanzania kuacha kusikilza na kusambaza kauli za kibaguzi znazotolewa na kiongozi huyo.

Majuma kadhaa yaliyopita Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tundu Lissu alitoa kauli za kukosa maamuzi ya serikali huku akimtaja Rais wa Jamhuri ay Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akidai kuwa anafanya maamuzi ya kuwakandamiza watanzania Bara kwa kuwa ametoka upande wa Pili wa Muungano,  Tanzania Zanzibar

Vyama vilivyotoa tamko hilo ni ADA TADEA, CCK, NLD, Demokrasia Makini, NCCR- MAGEUZI, TLP, UPDP, SAU, UMD, NRA na Chama cha DP.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS