Header Ads Widget

VIJANA JIEPUSHENI NA MATUMIZI MABAYA YA MITANDAO YA KIJAMII- BRIGEDIA JENERALI CHARLES FERUZI


 Vijana wametakiwa kujiepusha na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ili kuepuka madhara yanayoweza patikana kutokana na matumizi mabaya huku wakiendelea kuwa na uzalendo kwa nchi yao  ikiwemo kuilinda amani iliyopo kwa kufanya kwa kuwa mfano mzuri wa kuigwa


 Hayo yameelezwa na Mgeni rasmi Brigedia Jenerali Charles  Feluzi wakati wa kufunga mafunzo ya awali  katika Kikosi 843 JK wilayani Nachingwea mkoani Lindi ambapo amewataka vijana  hao  waliohitimu  Mafunzo kujiepusha na matumizi kabaya  ya mitandao ya kijamii kutokana na utandawazi uliopo .

Awali akiwasilisha taarifa ya mafunzo  mkuu wa Kikosi 843JK Nachingwea Mkuu wa kikosi Luteni Kanali Nyagalu Michael Malecela  amesema mafunzo hayo ya awali kwa vijana hao  wa kujitolea yamefanyika kwa muda wa miezi minne huku akiwaasa juu ya kuwa wazalendo pamoja na kuendelea kuwa vijana bora kwa kutojihusisha na vitendo viovu. 

Kwa upande wake katibu tawala wilaya ya Nachingwea Haji Mbarouk Balozi aliwataka vijana kutumia fursa ya mitandao ya kijamii kwa faida na manufaa yao na sio kutumia vibaya mitandao hiyo

Baadhi ya vijana  waliomaliza Mafunzo ya awali  wamemshukuru Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwapatia fursa mbalimbali hasa ya kupata mafunzo hayo kwani  yamewaongezea ujuzi na kuwafanya kuwa wazalendo katika nchi yao. 

Jumla ya vijana  562 wa kujitolea wamehitimu Mafunzo ya awali katika kikosi 845JKT Itaka na kuwafanya kuingia awamu ya pili ya kupata mafunzo mengine.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI