Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Dkt. Elirehema Joshua Doriye kuwa Kamishna wa Uhifadhi, Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro (NCAA)
Dkt. Doriye anachukua nafasi ya Richard Rwanyakaato Kiiza, ambaye aliondolewa katika nafasi hiyo Machi 15, 2024
Aidha, Christopher Derek Kadio ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali. Anachukua nafasi ya Esther Hellen Lugwisha aliyemaliza muda wake.
0 Comments