Header Ads Widget

TANROAD YAREJESHA MAWASILIANO YA BARABARA YA MWEMBE-MYAMBA-NDUNGU.



NA WILLIUM PAUL, SAME. 

SERIKALI  mkoani Kilimanjaro  kupitia wakala wa barabara nchini (TANROADS)  imekarabati barabara  ya  ya Mwembe-Myamba -Ndungu yenye urefu kilomita 90.19  kwa kiwango cha Changarawe   kwa thamani ya  bilioni 1.6.


Mapema mwaka jana kupitia mvua    za Eli-Nino barabara  hiyo ilikata mawasiliano baada maporomoko  ya ngema na Miamba(mawe Makubwa) kutoka upande wa milimani.



Akizungumza  mkuu wa mkoa Kilimanjaro Nurdin Babu katika ziara ya kawaida  ya kukagua miundombinu  kutokana na mvua zinazoendelea hapa nchini


"Hii barabarani ni muhimu kwa  maslahi mapana ya wananchi wa wilaya ya Same   hasa wakulima wa tangawizi hivyo ililazimika kurudisha mawasiliano kwa haraka zaidi..



Mimi mwenyewe nilikuja nikakwama huku nikalazimika kutumia njia mbadala ambayo ni mbali  na sio wananchi wote wanaweza kufika kwenye njia hiyo,"Alisema Babu 


Aidha  Mkuu wa kitengo  cha matengenezo  ya barabara TANROADS  mkoa wa Kilimanjaro,   Mhandisi Benitho Nikodemu    alisema maeneo 18  ya barabara  hiyo yalikuwa  mito  inapita na makorongo  jambo ambalo yalisabisha kumeguka na ngema kuanguka barabarani.



 Mhandisi alisema  matengenezo   yaliyofanyika  ni pamoja na kuchonga barabara (Heavy  Grading) urefu wa kilomita15 na kuweka changarawe na  kupasua miamba .


Alisema "Tulipanua barabara  maeneo finyu  yaliyotokea ufa kwenye tuta la barabara  kujaza  mawe  makubwa(Rock  boulders)maeneo  yaliyokatika na kujenga mitaro na kuta za mawe na kazi hii ilifanyika kwa haraka  kutokana na mkandarasi kuwa na vifaa vingi na vya  kuaminika,"alisema Mhandisi.


Aidha mkandarasi anayefanya matengenezo katika barabara hiyo mhandisi Baliunmn Mathias  kutoka kampuni JP Traders alisema mradi huo umekamilika kwa asilimia 95 na kuomba mwezi moja ili kumalizia maeneo yaliyobakia na kufanya marekebisho watakayomaliza.


"Kwa sisi ni kama tumemaliza kwa sasa tunasubiri kukamilisha asilimia  5 iliyobaki pamoja na kupokea maelekezo tutakayoelekeza  ili kuongeza ufanisi,"alisema.

Mwisho.. 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS