Header Ads Widget

BILIONI 1.3 KUDHIBITI MAFURIKO KILOSA

Na Ashton Balaigwa,MOROGORO

SERIKALI imetoa Sh bilioni 1.3 kwa Wilaya ya Kilosa iliyopo Mkoani Morogoro,kwaajili ya  kufanya utekelezaji wa miradi ya Dharua ya ujenzi wa mifereji ya kisasa, miundombinu ya Barabara za vijiji na kuboresha kingo za mito ili  kumaliza tatizo la  mafuriko ya mara kwa mara yanatokea katika wilaya hiyo kongwe ya  Kihistoria.


Akizungumza wakati ukaguzi na  kutembelea miradi hiyo huku akiongozana na Kamati ya Siasa Chama cha Mapinduzi (CCM)  Wilaya hiyo kama utekelezaji wa Ilani Mbunge wa Jimbo la Kilosa Profesa Paramagamba Kabudi,amesema tayari serikali alisema  fedha hizo zitasaidia kuimarisha miundombinu ambayo awali ilikuwa haipo na kusababisha maji  kuingia kwenye nyumba za wananchi na kusababisha mafuriko.

 Profesa Kabudi amepongeza hatua hiyo ya  serikali ya kutoa fedha hizo na kwamba  sasa itakuwa mkombozi kwa wakazi wa Kilosa kwani kwa muda mrefu wamekuwa wakiathiriwa na mafuriko hayo hata pale mvua zisiponyesha katika wilaya hiyo na kunyesha mikoa mingine kutokana na mito mingi kupita katika wilaya hiyo.


“ Kwa dhati kabisa namshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutupatia fedha hizi kwaajili ya ujenzi wa miundombinu ikiwemo mifereji ya kisasa kabisa ,hii itatusaidia kuondokana na hali ya mafuriko”alisema Mbunge Profesa Kabudi….

Amesema Jiographia ya mji wa Kilosa imezungukwa na Milima na mito mikubwa, hivyo imekua ni vigumu kuepukana na mafuriko tangu enzi za wakoloni hawa hivyo ujenzi wa miundombinu hiyo itasaidia kumaliza tatizo hilo la mafuriko.


 “ Sasa historia inakwenda kuandikwa, Baada ya Serikali kutenga zaidi ya shilingi bilioni 1.3 ili kujenga mifereji ya kisasa katika maeneo hatarishi” amesema Kabudi


Akizungumzia mkakati wa wilaya hiyo kuondokana na mafuriko hayo, Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara wa Vijijini na Mijini(Tarura)wa wilaya ya Kilosa,Mhandisi Wiston Munyaga,amesema kuwa fedha hizo zitajenga mifereji   ili kuondoa adha ya maji yanayotokana na mito mbalimbali  inayosababisha  mafuriko yanaingia kwenye makazi ya watu.


Naye Diwani wa Kata ya Mvumi wilayani humo,Shaban Malingo,meisema mafuriko yanayotokea wilayani yamekuwa yakigharimu maisha ya watu pamoja na makazi yake.


Mwisho

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI