Header Ads Widget

UVCCM KUWASHUGHULIKIA WATAKAOJITOKEZA NDANI YA CHAMA KUCHUKUA FOMU KUGOMBEA NAFASI YA URAIS 2025.

 



JUMUIYA ya Umoja wa vijana Uvccm imesema itawashughulikia  watakaojitokeza ndani ya chama cha mapinduzi CCM kuchukua fomu kugombea nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu 2025.


Jumuiya hiyo imewaomba  wanaccm kumuachia Mhe.Rais ambae ni Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais Dk,Samia Suluhu Hassan awe mgombea pekee atakaepeperusha bendera ya CCM  ngazi ya urais katika uchaguzi huo.


Akizungumza na wananchi wilayani kilolo mkoani Iringa katika mkutano wa hadhara wa  uzinduzi wa kampeni ya ‘’jiandikishe  chagua ccm’uliofanyika kata ya Nyalumbu, mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Taifa Muhsin Ussi  alieleza kuwa kutokana na kazi na kasi kubwa ya maendeleo inayofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya  uongozi wake Dk.Samia Suluhu Hassan hakuna sababu ya  mwanccm kujitokeza kuchukua fomu ya kugombea urais.


Alisema katika nafasi ya Rais vijana wa UVCCM wameweka msimamo wao kuwa fomu itakayotoka ni moja ambayo ataichukua Dk.Samia hii inatokana na kazi kubwa anayoifanya katika kipindi  kifupicha miaka mitatu.


Alisema atakaethubutu kuchukua fomu ataiona rangi  ya umoja wa vijanawa CCM  unaoongozwa na Mwenyekiti wake   Mohamed Kawaida akajitokeza kuchukua fomu.


Akimkaribisha Mgeni rasmi,Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Iringa Agrey Tonga alieleza kuwa vijana wote wenye sifa na vigezo wajitokeze kwa wingi kuchukua fomu kugombea katika uchaguzi wa Serikali za mitaa.


Toga alieleza kuwa UVCCM itawaunga mkono vijana wote watakaogombea katika uchaguzi huo na uchaguzi wa Serikali za mitaa ili  kujenga uwakilishi wa vijana katika maamuzi ya  Taifa na kuleta maendeleo endelevu.


Nae Mwenyekiti wa  uvccm wilaya ya kilolo  Amani Mdeka alisema kuwa  Uvccm imejipanga kuhakikisha  katika uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajia kufanyika mwaka huu  chama cha Mapinduzi CCM kinashinda kwa kishindo mitaa yote.


MWISHO.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI