Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina Mndeme leo
Jumanne Februari 27,2024 amekutana na kuzungumza na wafanyabiashara wa Sukari ili kubaini sababu
inayochangia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.
Wafanyabiashara aliokutana nao Mkuu wa Mkoa ni
pamoja na wenye viwanda vya Sukari,mawakala pamoja na wenye maduka ya jumla na
rejareja,ambao wametaja sababu mbalimbali zinazosababisha upungufu wa sukari
Wafanyabiashara wenye maduka ya jumla na rejareja
wametaja sababu mbalimbali zinazowafanya kupandisha bei ya sukari ikiwemo
gharama kubwa wanayonunulia kutoka
viwandani.
Akizungumzia changamoto ya Sukari Meneja wa kiwanda
cha Sukari cha Kagera Sugar kanda ya ziwa Bwana Hassan Burhan Abdulkarim
amesema Mvua za El-nino zimesababisha uzalishaji kushuka kutokana na mitambo
kushindwa kuingia kwenye mashamba baada
ya kujaa maji.
“Suala
la changamoto ya Sukari ni tatizo la kiukanda misimu hii miwili mitatu nyuma
Mvua zimenyesha nyingi sana kupita kiasi ambazo Mvua hizo zimepelekea Mashamba
kujaa Maji na Mashamba yakishajaa Maji Mashine zile za kupakia na Trekta za
kutoa Mua ndani ya Shamba kupeleka kiwandani kwa ajili ya kusaga haziwezi
kuingia tena mashambani, lakini Sukari inahitajika ni kipi kifanyike tufunge
kiwanda au tutafute mbadala mbinu mbadala ni kubeba Mua begani kampuni imefanya
hizo jitihada imeshaajili zaidi ya watu elfu saba kwa ajili ya kubeba Mua ndani
ya Shamba mpaka kwenye kiwanda”.amesema
Meneja Hassan
Wafanyabiashara hao wameishauri serikali kuhakikisha
inakuwa na utaratibu wa kuweka akiba ya kutosha ya bidhaa hiyo kabla ya uhaba kutokea ikiwa ni pamoja na
ushirikishaji wadau kwenye upangaji wa bei ya sukari.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Mhe. Christina
Mndeme amesema serikali kwa kutambua umuhimu wa bidha hiyo kwa wananchi wa Mkoa
wa Shinyanga itashughulikia changamoto ya upungufu wa Sukari inayosababisha
kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.
“Tunamuangalia
yule mwananchi wa chini mkulima wa chini je anaweza kumudu shilingi elfu nne
shilingi elfu tano kwa kilo moja ya Sukari ebu fikiria kilo moja ya Sukari kwa
familia ya kawaida ni watu 8, Sukari ni muhimu sana kwetu Sukari siyo anasa
Sukari siyo sterehe Sukari ni bidhaa muhimu na hasa katika kipindi hiki cha
Kwarezima na tunapoenda kwenye mwezi mtukufu lakini pia kwa matumizi yetu ya
kawaida ya nyumbani niseme tu kwamba maoni na ushauri wetu nimeupokea ninaomba
mniachie niufanyie kazi”.amesema RC Mndeme
Kikao hicho kimehudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mkuu wa Wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi, Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Mkude pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita.
Aidha siku chache zilizopita Matukio Daima ilizungumza na baadhi ya
wafanya Biashara wakiwemo mama lishe Mkoani Shinyanga,ambao waliitaka serikali
kuchukua hatua za haraka kutatua changamoto ya upungufu wa Sukari ambayo
imechangia kuwepo kwa mfumko wa bei.
Walieleza kuwa hivi karibuni bei
ya Sukari imepanda kutoka elfu 2800 hadi elfu nne (4000) kwa kilo moja na
kwamba upatikanaji wake ni mgumu.
Wafanyabiashara walisema hatua hiyo imechangia kupungua kwa wateja na kuathiri mapato katika Biashara zao za kila siku huku wakiiomba serikali kushughulikia changamoto hiyo haraka ili kuondoa usumbufu unaojitokeza.
Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akizungumza kwenye kikao chake na
wafanyabiashara wa Sukari Mkoani Shinyanga Februari 27,2024.
Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga Mhe. Christina Mndeme akizungumza kwenye kikao chake na
wafanyabiashara wa Sukari Mkoani Shinyanga Februari 27,2024.
0 Comments