Header Ads Widget

MBUNGE CONDESTER ATEMBELEA ENEO LENYE MADINI YA SODA KITE


Na Ibrahim Yassin Matukio App -Songwe 

Mbunge wa Jimbo la Momba,  Condester Sichalwe (Mundy) aongoza timu ya wataalamu akiwemo  Afisa Madini mkazi Mkoa wa Songwe Chone Malembo kwenda kushuhudia utafiti wa madini ya Sodalite yaliyobainika eneo jimboni kwake Kijiji Cha Chindi.



 Mbunge Condester  amempongeza mchimbaji mdogo wa madini ya Sodalite Nicko Laus Buseni kwa kuamua kufanya utafiti wa madini hayo ndani ya Jimbo lake na kueleza kuwa yupo tayari kumuunga mkono, ikiwa ni pamoja na kumkutanisha na taasisi za kifedha ili apatiwe Mkopo.


Condester  amewasihi wananchi wa kijiji cha Ntinga na Momba kwa ujumla kuchangamkia fursa ya kupata leseni kwa ajili ya uwekezaji wa madini ya Sodalite amb ayo yanadaiwa kugundulika kijiji cha Chindi Kata ya Msangano.

Afisa Madini Mkazi mkoa wa Songwe, Chone Male mbo, amesema madini ya Sodalite yanafanyiwa utafiti kijiji cha Chindi Kata ya Msa ngano Wilaya ya Momba, yatakuwa ni madini mapya kupatikana ndani ya Mkoa huo, kwani hakuna eneo jingine  yanayopatikana  madini hayo  ndani ya Momba.


Mkoa wa Songwe ni miongoni mwa mikoa yenye fursa za madini yakiwemo madini adimu  hivyo ipo haja vijana kuchangamkia fursa za uchimbaji kuongeza kipato.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI