Kama unaishi mikoa ya Morogoro, Lindi, Iringa, Mtwara, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma basi kaa mguu sawa kwani Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa angalizo ya uwepo wa hali mbaya ya hewa kwa siku tano.
Utabiri huo unakuja siku chache tangu baadhi ya mikoa kama Dar es Salaam na Morogoro kushuhudia mvua kubwa iliyoathiri miundombinu na kusababisha vifo.
Utabiri huo wa TMA umetolewa leo Januari 29,2024 utaanza kesho Januari 30 na utadumu hadi Februari 2 mwaka huu.
“Angalizo la mvua kubwa limetolewa katika maeneo machache ya mikoa ya Morogoro, Lindi, Mtwara, Iringa, Mbeya, Songwe, Njombe na Ruvuma,”iliandikwa taarifa hiyo.
Wakazi katika mikoa hiyo watashuhudia athari ya makazi yao kuzungukwa na maji, pamoja na kuathirika kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi.
0 Comments