Header Ads Widget

WATU 14 WAFARIKI KWA AJALI YA GARI LINDI

 

NA HADIJA OMARY, LINDI 

Watu 14 wamepoteza maisha na wengine 26 kujeruhiwa kufuatia ajali ya Basi la kampuni ya Baraka lenye namba ya usajili T336 DPW lililokuwa linatokea Wilayani Newala Mkoani Mtwara  kuelekea jijini Dar es salaam   kufeli breki na kuanguka  katika eneo la Mputa maarufu kama kona ya Nyale,katika Halmashauri ya Mtama Mkoani Lindi


Akizungumza  leo Jumapili Novemba 26.2023,kamanda wa polisi Mkoa walindi ACP  John  Makuri amesema kuwa ajali hiyo imetokea majira ya saa1:10 Asubuhi ya leo ambapo dereva wa Kampuni ya BARAKA CLASSIC lenye namba za usajiliT336DPW, gari lilikuwa linatokea Newala kwenda Dar es Salaam

 

Kamanda amefafanua kuwa vifo 12,vilikuwa vya abiria waliokuwa ndani ya basi hilo huku vifo vya watu wawili walikuwa Watembea  kwa miguu,na majeruhi 26,wanapatiwa matibabu katika hospitali ya nyangao


"Watu hao 14 waliofariki,12 ni abiria waliokuwa wanasafiri na basi hilo ,na wawili walikuwa Watembea  kwa miguu,dereva wa basi la baraka anapatiwa matibabu,katika hosptali ya Nyangao akiwa chini ya ulinzi".Amesema kamanda Makuri

Pia kamanda Makuri ametoa wito kwa madereva ambao wazembe,nakusema kuwa sheria kali zitachukuliwa dhidi ya madereva wazembe ambapo amesema kuwa ,madereva wanadhamana kubwa ya maisha ya abiria ambapo pia amesema  dereva alikuwa anajua kama gari lina hitilafu lakini bado alikubali kuendesha.


Moja ya mashuhuda wa ajali hiyo Juma Machalila amesema wakati wa zoezi la uokoaji walitokea nyuki na kulifanya zoezi la uokoaji kuwa gumu kutokana na nyuki hao.

"Nyuki hao wapo siku zote ila baada ya kutokea ajali walianza kung'ata watu nakuanza kukimbia tukalazimika kununua dawa ya wadudu (dawa ya rungu) pamoja na kuchoma matairi ,vifo vilivyotoÄ·ea ni sababu moja wapo ya watu kukosa msaada kwa haraka"amesema Machalila. 


Naye diwani wa kata ya Mtama halmashauri ya Mtama Maria Nyale amesema kuwa gari hilo lilikuwa limefeli breki na kwenda kusababisha watu zaidi ya 14 kufariki.

"Tukio kubwa lililo tokea baada ya ajali kutimka kwa nyuki,walitimka sana ikasababisha kushindwa kuwaokoa watu lakini polisi walifika mapema wakashirikiana na wananchi kuchoma mipira nyuki wakatoka na zoezi la uokoaji likaendelea ,ambapo watu 14 wamefariki  "amesema Nyale. 


Nae Mkuu waMkoa wa lindi Zainabu Telack,amewashukuru wananchi waliosaidia kuokoa pindi ajali ilipotokea ambapo baada ya kutokea ajali nyuki wengi walitokea na kusababisha baadhi ya wananchi kuumwa na nyuki  na kupelekwa hosptali.


"Niwashukuru sana wananchi wa Mtama kwa juhudi mliofanya ya uokoaji pindi ajali ilipotokea  licha ya kwamba kulikuwa na nyuki wengi"Amesema Telack

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI