Header Ads Widget

SERIKALI MUFINDI YAONYA MIMBA KWA WANAFUNZI





SERIKALI  ya  wilaya ya  Mufindi  mkoani  Iringa  imesema  itawachukulia  hatua  kali   wazazi  wa  wanafunzi watakaobainika  na  mimba   pindi  shule zitakapofungua  mwakani 2024.

Kuwa  hivi  karibuni  shule  zote  na msingi na sekondari  zinakwenda  kufungwa  kwa  ajili ya  wanafunzi  kwenda  rikizo ndefu ya  mwezi  zaidi ya mmoja  hadi hapo  mwakani kama  itakapotangazwa na  wizara   husika  hivyo  kwa  kuwa   hadi  sasa  wanafunzi  wamelelewa  vyema  shuleni kwa  kuwa salama  pasipo  kuwa na mimba ni  vizuri  wazazi  kuwalinda  watoto  wao kwa muda  ambao  wakakuwa nao  nyumbani  wakati  wa  likizo.


Mkuu  wa  wilaya ya  Mufindi Dkt  Linda Selekwa aliyasema  hayo juzi  wakati  wa mahafali ya  nane  katika  chuo cha ufundi  standi Rural  Development  Organization (RDO)  Mdabulo alisema  hadi  hivi  sana  kwenye  tarafa  ya  Ifwagi  hakuna  taarifa  ya  mimba  za  wanafunzi mashuleni  jambo  ambalo linaonesha  kwa kiasi  kikubwa  jinsi  ambavyo  walimu  walivyowewza  kulinda  vema  watoto kwa  wakati  wote  wa masomo shuleni.

Hivyo  ni  wajibu  wa  wazazi    kuhakikisha   wakati  huu  wa  likizo ndefu ya  mwisho  wa  mwaka   wanabeba  dhamana  ya  kulinda  watoto  wao  ili  shule  zitakapofunguliwa   watoto hao  warudi  mashuleni   wakiwa  salama  bila  ya  mimba.

Alisema  hadi  sasa  pamoja na kata  ya Mdabulo na  Ifwagi  kutokuwa na  taarifa  za  mimba  za  wanafunzi  ila  kuna  baadhi ya  maeneo kwenye  kata na  tarafa  nyingine  zimekuwepo  taarifa  za  mimba  za  wanafunzi  na wahusika  wote  wa  mimba  hizo   wamekwisha  chukuliwa  hatua kwa  kufikishwa mahakamani  .

 Hivyo  alisema  kama  serikali ya  wilaya  isipenda  kuona   wanafunzi  wanakatishwa  ndoto  zao na masomo  kutokana  na mimba  na  kuwa  wahusika  wa mimba  za  wanafunzi   hawatafumbiwa  macho na hata kama  mwalimu  atabainika  kuhusika  atachukuliwa hatua  kali  za  kisheria.

 " Ninachowaomba   wazazi   kuwalinda  watoto  wetu na kutowaficha  wale  wanaosababisha   watoto  wetu  kutotimiza  ndoto  zao na  kupata  elimu  wafichueni  wahusika  na mimba  ila sheria  ichukue mkondo  wake  hakuna haja ya  kuwaficha  hao  sil watu  wema  hata  kidogo ikibainika  mzazi  umemficha mhusika  wa mimba  za wanafunzi  wewe  ndio  utabeba  dhamana  ya  kufikishwa  mahakamani "  alisema 



Dkt  Selekwa ambae  ndie  alikuwa  mgeni  rasmi katika  mahafali  hayo  aliwakilishwa na  katibu  tawala  wa  wilaya ya  Mufindi Frank Sichalwe   alisema  kuwa   serikali ya  awamu ya  sita  chini ya  Rais  Dkt  Samia  Suluhu  Hassan  ameendelea  kugharamia  elimu   bila malipo  lengo   kuwezesha  kila mtoto  wa mtanzania  kupata  elimu  pasipo  kisingizio  cha  kukosa ada  .

Kuwa  kutokana na jitihada  hizo za Rais Dkt  Samia  ni  vizuri  kila mmoja  wetu  kuunga mkono  kwa  kuhakikisha  hakuna  mtoto  anyekatishwa masomo kwa  kisingizio   chochote  na  wale  wanaosababishiwa  kukatisha masomo kwa sababi zinazozuilika  za mimba  basi  waliohusika na sababu  hizo  wanapaswa  kuwajibishwa  vikali .

Pia  alisema  hata  kwa wanafunzo  wanaosoma   vyuo  mbali  mbali  zikiwemo  vya  ufundi pia  wanapaswa  kulindwa  dhidi ya  mimnba   ili  kutimiza ndoto  zao  za  kumaliza mafunzo  salama  kwani  alisema  pamoja na  serikali  kugharamia  elimu ya msingi na  sekondari  imekuwa   ikigharamia  elimu ya  vyuo  vya  ufundi  kwa  kufadhili  masomo  ya muda  mfupi  kwa   wanafunzi  wenye  uhitaji na  shabaha  ni kuona   vijana  wenye  ndoto ya  kuja kuwa mafundi  wanawezeshwa  hivyo  si sawa  kama  ndoto  zao  zitavurugwa na mtu .

Katika hatua  nyingine  alisema  kuwa  serikali  wilayani  Mufindi  imeendelea  kuweka  mfumo  mzuri  wa  wakulima  kupata  mbole ya  Ruzuku kwa  wakati na tayari  mbolea  zimeanza  kusambazwa  ili  kuwezesha   wakulima  kutumia  mvua zinazotarajia  kuanza  kunyesha  kwa kilimo .

Alisema ni wajibu  wa kila  mmoja  kuanza maandalizi mapema ya mashamba  na  kwa  wale  vijana  wanaoshinda   vijiweni  wanapaswa  kutambua  kuwa  kufanya   hivyo  ni kosa na  iwapo  watakutwa   vijiweni  muda  wa  kazi  watawajibishwa  pia  .


Akizungumzia  kazi  mbali  mbali  zinazofanywa na  chuo  hicho  cha RDO  Mdabulo  alisema  kuwa kwa  upande wa  serikali ya  wilaya ya  Mufindi  inathamini  mchango  mkubwa  wa  chuo  hicho  hasa katika  kuhudumia  jamii inayokizunguka  chuo kwa  kuanzisha miradi ya maji  safi  na  salama   pia  vijana  kuwa na ujuzi  mkubwa wa  kutengeneza  bidhaa mbali  mbali  .

 Hivyo kwa ajili ya kuunga mkono  jitihada za  chuo  serikali ya willaya ya  Mufindi itaendelea  kuhimiza  wazazi  kulipa ada kwa  wakati pia  kuona  inaunga mkono  jitihada za  chuo  hicho kwa  kununua bidhaa zinazozalishwa na  wanafunzi  hao  zikkiwemo batiki na  bidhaa nyingine .

Akizungumza  kwa niaba ya  mkurugenzi  wa RDO  Fidelis Filipatali  mwakilishi wa  mkurugenzi huyo  Obadia Ngailo  alisema  kuwa  chuo  hicho kimefanikiwa kusajili wanafunzi wa kozi za muda mfupi wapatao 42 wavulana 31 na wasichana 11 pia  kusimamia nidhamu ya wanafunzi na watumishi na kuchukua hatua stahiki inapojitokeza masuala ya utovu wa nidhamu.

Pia  wamefanikiwa kuongeza vyanzo vya uzalishaji mfano nyuki, na ng’ombe wa maziwa, hivyo kuongeza pato la chuo na kuongeza ufanisi kwa wanafunzi wa fani ya kilimo na ufugaji ,wamefanikiwa kuhamasisha wanafunzi kufanya kazi za mikono kwa ajili ya kujifunza kwa vitendo zaidi na kuongeza kipato cha idara.

"Tumefanikiwa kununua shamba la idara lenye takribani ekari 60 kwa mapato ya ndani ya idara ili kuendesha shughuli za ufugaji na kilimo tumefanikiwa kuanzisha mgahawa kwa ajili ya watumishi na wanafunzi ili kutoa huduma ya chakula na kuongeza mapato ya idara pia kuongeza ujuzi kwa wanafunzi wa upishi na wamefanikiwa  kupata tenda mbali mbali toka jamii inayotuzunguka na tenda za serikali kama vile kujenga Zahanati, madarasa, kutengeneza madawati na kuandaa vyakula vya wageni mbali mbali katika maeneo yanayotuzunguka "


Ngailo  alisema  kuwa wamefanikiwa na tunaendelea kuandaa na kufanya semina na warsha mbali mbali kwa watumishi na wanafunzi wa vyuo vyetu, zikiwemo semina za ujasiriamali mifumo wa ufundishaji na warsha inayohusu matumizi bora ya ardhi (PERMACULTURE)Kwa kushirikiana na ofisi ya TEHAMA.

Alitaja  changamoto  zinazokabili  chuo  hicho  kuwa ni Kukosekana kwa nyumba za watumishi hali inayofanya baadhi ya watumishi kutembea umbali mrefu na wengine kuishi mazingira ambayo si  mazuri pia kukosa viwanja vya michezo mbali mbali kama vile, mpira wa miguu, mpira wa pete pamoja na Uhaba wa madarasa hasa kwa fani ya ujenzi na ufundi magari.

MWISHO 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI