Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
MJUKUU WA HAYATI MWALIMU JULIUS NYERERE ALIYEKUWA ANAISHI SHINYANGA KUZIKWA KESHO BUTIAMA MKOANI MARA
MJUKUU WA HAYATI MWALIMU JULIUS NYERERE ALIYEKUWA ANAISHI SHINYANGA KUZIKWA KESHO BUTIAMA MKOANI MARA
Misalaba
Monday, November 13, 2023
Mwenyekiti wa mtaa wa Mabambase Bwana Seif Nassor Hemed akizungumza.
Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Mwili wa Edward Majige Nyerere ambaye ni Mjukuu wa Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius kambarage Nyerere umesafirishwa leo kwenda Butiama Mkoani Mara kwa Mazishi.
Marehemu Edward Nyerere mwenye umri wa Miaka 26, alifariki dunia juzi siku ya jumamosi Novemba 11,Mwaka huu 2023 kwa ajali ya pikipiki aliyokuwa akiendesha,iliyotokea majira ya saa 12.00 asubuhi katika Barabara ya Uhuru eneo la Bushushu.
Edward Nyerere alikuwa mtumishi wa NIDA Mkoa wa Shinyanga ambaye alikuwa akiishi Mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi katika Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza mwenyekiti wa mtaa wa Mabambase Bwana Seif Nassor Hemed ambaye ameelezea namna alivyopokea taarifa za tukiola kifo cha marehemu huyo.
Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi wameomba watumiaji wa vyombo vya moto kuhakikisha wanazingatia sheria na kanuni za usalama barabara ikiwa ni pamoja na kuepuka mwendo kasi.
Mazishi ya Edward Nyerere yanatarajiwa kufanyika kesho Jumanne Novemba 14,2023 katika kijiji cha Butiama Mkoani Mara,mahali alipozaliwa.
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
KIKUNDI CHA WAMANDA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MAONO YAKE
Gasper
Monday, December 15, 2025
Kikundi cha Akinamama wanaonufaika na Mikopo ya asilimia kumi ya Halmashauri cha Wam…
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
TANZIA :FILICIAN CHAULA AFARIKI DUNIA
Monday, December 08, 2025
MEZA YA MAGAZETI JUMANNE DISEMBA 9/2025: MIAKA 64 YA UHURU :TAIFA LINAENDELEA KULILIA GAVABA BoT ,IGP,AG MWANAMKE..
Monday, December 08, 2025
MKE WA BALTASAR WA VIDEO 400 ZA NGONO ,VIDEO YAKE YANASWA NA MUME MWINGINE
Saturday, November 09, 2024
Contact form
0 Comments