Home
About
Contact
Header Ads Widget
Home
News
Entertainment
Sports
Magazeti
Home
kitaifa
MJUKUU WA HAYATI MWALIMU JULIUS NYERERE ALIYEKUWA ANAISHI SHINYANGA KUZIKWA KESHO BUTIAMA MKOANI MARA
MJUKUU WA HAYATI MWALIMU JULIUS NYERERE ALIYEKUWA ANAISHI SHINYANGA KUZIKWA KESHO BUTIAMA MKOANI MARA
Misalaba
Monday, November 13, 2023
Mwenyekiti wa mtaa wa Mabambase Bwana Seif Nassor Hemed akizungumza.
Na Mapuli Misalaba, Shinyanga
Mwili wa Edward Majige Nyerere ambaye ni Mjukuu wa Baba wa Taifa hayati Mwalimu Julius kambarage Nyerere umesafirishwa leo kwenda Butiama Mkoani Mara kwa Mazishi.
Marehemu Edward Nyerere mwenye umri wa Miaka 26, alifariki dunia juzi siku ya jumamosi Novemba 11,Mwaka huu 2023 kwa ajali ya pikipiki aliyokuwa akiendesha,iliyotokea majira ya saa 12.00 asubuhi katika Barabara ya Uhuru eneo la Bushushu.
Edward Nyerere alikuwa mtumishi wa NIDA Mkoa wa Shinyanga ambaye alikuwa akiishi Mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi katika Manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza mwenyekiti wa mtaa wa Mabambase Bwana Seif Nassor Hemed ambaye ameelezea namna alivyopokea taarifa za tukiola kifo cha marehemu huyo.
Baadhi ya wakazi wa Mtaa wa Mabambasi kata ya Ndembezi wameomba watumiaji wa vyombo vya moto kuhakikisha wanazingatia sheria na kanuni za usalama barabara ikiwa ni pamoja na kuepuka mwendo kasi.
Mazishi ya Edward Nyerere yanatarajiwa kufanyika kesho Jumanne Novemba 14,2023 katika kijiji cha Butiama Mkoani Mara,mahali alipozaliwa.
Post a Comment
0 Comments
MAGAZETI
NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI
TV News
World News
UZA NUNUA NASI LEO
Subscribe Us
MATANGAZO
TIBA YA UKANDAJI WA MGONGO, KICHWA KUTOKA NEEMA BEAUTY, SPA SALOON
MAKALA NZURI ZAIDI
FURSA SEKTA YA MKONGE, WANANCHI WAITWA BANDA LA TSB NDANI YA SABASABA
Andrew Chale
Friday, July 04, 2025
Na. Andrew Chale, Matukio Daima App Dar Wananchi wameaswa kuchangamkia fursa ilizopo …
STAY CONNECTED WITH US
Ad Space
Responsive Advertisement
Most Popular
MAUAJI YA MWANAMKE IRINGA ,WAKILI AMBINDWILE AONYA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI
Monday, June 30, 2025
MEZA YA MAGAZETI LEO JUMAMOSI JUNI 28/2027: KISHINDO CHA RAIS SAMIA AKIHITIMISHA SHUGHULI ZA BUNGE ,FOMU KWA WAGOMBEA KUANZA KUTOLEWA LEO,USAJILI MBIO ZA GREAT RUAHA MARATHON UNAELEKEA UKINGONI JISAJILI LEO
Saturday, June 28, 2025
MEZA YA MAGAZETI LEO JULAI 1/2025:RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU ITALI ABARIKI UJENZI WA WODI YA AKINA MAMA TOSAMAGANGA,MBIO ZA GREAT RUAHA BADO SIKU 3 KUFANYIKA NI JUMAMOSI HII JISAJILI SASA..
Tuesday, July 01, 2025
Contact form
0 Comments