Header Ads Widget

CCM IMVUE UBUNGE PAULINA GEKUL -ASASI ZA KIRAIA


Na Matukio Daima App 


BAADA  ya  Rais  wa  jamhuri ya  Muungano  wa  Tanzania  Dkt  Samia  Suluhu Hassan kutengua  uteuzi  kwa  aliyekuwa  naibu  waziri  wa katiba  na  sheria   Paulina  Gekul ,mashirika   yasiyo kuwa  ya  kiserikali  mkoani Iringa  yamempongeza  Rais  Samia  kwa  uamuzi  wake  mzuri  huku yakitaka  chama  cha mapinduzi (CCM) kuchukua  hatua  za  kuunga mkono hatua  hiyo kwa  kumvua ubunge na uanachama Gekul .

Raphael Mtitu katibu mtendaji asasi ya ICISO Iringa 

Wakizungumza  na Matukio Daima Media katibu  wa  shirika  lisilo la  kiserikali la  ICISO mkoani  Iringa Raphael  Mtitu na katibu  mtendaji  wa  shirika  lisilo la kiserikali la  Caringi Hearts  (CAHE)  Jameda Kulanga   walisema  kuwa   hatua  iliyochukuliwa na Rais Dkt  Samia  imechukuliwa kwa  wakati mzuri na imezingatia  utawala   bora  na  wao kama  asasi za  kiraia   wanaungana na Rais  katika  hatua  hiyo  nzuri  iliyochukuliwa .


Mtitu  alisema  kuwa  baada ya  kupata  taarifa  ya naibu  waziri  huyo  kufanya  vitendo  vya uzalilishaji walipokea kwa  mtazamo touati  sana  hasa  kuona mtuhumiwa ni kiongozi  mwenye  jukumu kubwa  kwa  Taifa katika  kupinga  vitendo  vya ukatili wa kijinsia  nchini .

Hivyo  alisema kuwa   wao kama  wanaharakati  wa masuala la kupambana na ukatili  wa kijinsia nchini  walikuwa  wakisubiri  kuona  hatua  nzuri za  kiuwajibishaji kama  hizo  zikitolewa  japo kabla ya  Rais  kufikia uamuzi  wa  kutengua uteuzi  wake  walitarajia  naibu  waziri   huyo angejiwajibisha kwa  kujiuzulu nafasi  zake  zote  kupisha uchunguzi .


Alisema  kuwa  chimbuko la  unyanyasaji  huo  zinatajwa  kuwa ni ugomvi wa  kibiashara kati yake na mpiga kura  wake   jambo ambalo ni  kinyume na kazi  na  wajibu wa mbunge  na wapo  wabunge  wengine na  viongozi  wengi  wenye maslahi  kama  hayo majimboni ya   kugeuza majimbo yao kama  sehemu ya biashara  na  hivyo kupelekea migongano ya  kimaslahi  kati yao na  wapiga kura  wao .


"  Huyo mbunge  ama  diwani ni mwakilishi wa  wananchi  bungeni ama kwenye  vikao  vya baraza la madiwani  sasa kama   mwakilishi  wa wananchi anafanya  shughuli  zinazofanana na  wananchi  kwenye  eneo  alilochaguliwa ni chanzo  cha  vurugu kama  hizi  jambo ambalo  si  sawa  lazima  achague  moja  kati ya siasa ama  biashara  mbunge  lazima  awe na heshima  ya  wapiga kura  wake "


Mtitu  alisema  kuwa   ndio maana  kwenye  katiba mpya   wananchi  wengi  wanapigania kuona mbunge  hawi mali ya chama bali anakuwa mali ya wananchi  ili  kuweza  kumuwajibisha  pale anapokosea .

Alisema  kilichofanywa na mbunge   huyo ni  taswira ya  wazi  kuwa  kuna haja ya  kuwa na katiba  mpya  itakayomuwezesha  mpiga  kura  kumwajibisha mbunge  wake  moja kwa moja .

Hata  hivyo  alisema  kuwa  mbali ya kuwa  naibu  waziri  huyo  anatokana na chama  cha  siasa ni  vyema  chama  anachokiwakilisha   kumchukulia  hatua  kali  ikiwemo ya  kumchukuliwa hatua  za  kumsimamisha  ama  kumvua  uanachama   wakati  huu  wa  uchunguzi  wa  tuhuma  dhidi  yake .

"  Gekul  amechafua  sana  sifa  ya  chama  tawala  kwa  kutanguliza mambo  binafsi  na kuacha  misingi ya chama  hicho ambacho  kinajinasibu   kutetea  haki  za  binadamu  wote   sasa kama  Rais amechukizwa na  kuchukua  hatua tunasubiri  uamuzi wa chama  chake  kinachomdhamini nacho  kuchukua hatua  kama  kweli  kinaunga mkono uamuzi  uliochukuliwa  na  Rais  Dkt  Samia " alisema 


Mtitu  alisema  kuwa  iwapo  chama  chake  kinachomdhamini  ubunge  wake  lazima  kuchukua  hatua  za  haraka  kama  ambavyo  Rais alivyochukua  hatua  za haraka   dhidi ya  naibu   waziri  huo    kama  sehemu ya  fundisho  kwa   wabunge na viongozi  wengine .

Katika  hatua  nyingine  Mtitu  alisema kuwa  viongozi kama  Gekul  ndio  wamekuwa  kikwazo kikubwa katika mapambano  dhidi ya  ukatili wa kijinsia  nchini Tanzania  kwani  pale  ambapo  wanaharakati  wa kupinga  ukatili wa kijinsia wakipambana  kutokomeza ukatili wao  wamekuwa  chimbuko la  kuficha  uovu  ama kutetea kwa  kuwa na   wao ni  wahusika  wakuu wa ukatili kama  huo ndio maana  leo Mungu  ameamua  kumfichua Gekul ndani ya  siku  16  za  kupinga  ukatili wa kijinsia .


Kwa upande wake katibu mtendaji wa  shirika la CAHE Jameda Kulanga  alisema  kuwa  viongozi kama  hao  wanarudisha  nyuma  mapambano  dhidi ya ukatili  wa kijinsia  nchini kwani  walitegemea  kuona  viongozi  wanakuwa  mfano wa  kupinga  na  kukemea  ukatili wa kijinsia  nchini .

Hata   hivyo  alisema  hatua ya  kutumbuliwa kwenye nafasi yake  ya unaibu  uwaziri ni  nzuri na itawafundisha  viongozi   wengine  kutotumia  vibaya   vyeo  vyao  japo  bado  anashangazwa  kuona  hadi   leo  Gekul ni  mbunge  kimsingi  baada ya  kutenguliwa  nafasi hiyo kubwa  alipaswa  kujiuzulu  mwenyewe  kabla ya  kusubiri  kutumbuliwa hata  ndani ya  chama .


Wakati  huo  huo  wanaharakati  wa  kutetea haki  za binadamu  (Groundera)   chini ya kiongozi  wao  Deusdedith  Soka  wametoa tamko kwa  vyombo  vya habari  la kulaani  vitendo vya  kikatili   alivyofanyiwa   kijana  Hashimu  Ally  Philimon  Novemba 11 mwaka  huu   jimboni Babati mjini .

 Wanaharakati hao wamesema  wanalaani  unyama  huo  na kuomba   vyombo  vya  usalama  kufanya kazi  yake  ya  kuchukua hatua  dhidi ya  wahusika  wa  tukio   hilo  ili  iwe  fundisho  kwa  wengine .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI