Header Ads Widget

WAZIRI BASHE AAHIDI MAZURI KWA WAKULIMA KUHUSU SUALA LA MBEGU ZA KILIMO.

 

Mheshimiwa Hussein Bashe, Waziri wa Kilimo

Wananchi na wakazi wa eneo la Katesh Wilaya ya Hanang mkoani Manyara wafurika katika barabara kuungojea Msafara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassani ambapo Rais alipata wasaa wa kusikiliza kero zao.

Katika msafara huo wakazi wa Katesh watoa malalamiko yao juu ya upandaji wa bei za mbegu za kilimo kwa baadhi ya makampuni wakati maeneo mbalimbali nchini wakielekea katika msimu wa kilimo ambapo katika kulijibia hilo Rais Samia amsimamisha waziri wa Kilimo Mheshimiwa Hussein Mohamed Bashe kutoa ufafanuzi juu ya changamoto ya bei za mbegu za kilimo.

Kwa mujibu wa Waziri mwenye dhamana ya kilimo Mheshimiwa Bashe ametoa ufafanuzi wa jambo hili kwamba ameshawapa kazi maalum Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kuhakikisha ifikapo Oktoba 20 mwaka huu wawe wameshatoa bei elekezi ya mbegu hususani mbegu za mahindi kwa nchi nzima na kwa kila eneo.

Mheshimiwa Bashe amesikitishwa na kitendo cha baadhi ya makampuni yanayojihusisha na uzalishaji wa mbegu za kilimo, kuuza mbegu zao kwa gharama za juu kwani serikali inatoa maeneo, miundombinu na baadhi ya huduma za muhimu kuhakikisha makampuni haya yanazalisha mbegu kwaajili ya kuwasaidia wakulima na sio kuwakandamiza kwa namna moja ama nyingine.

Aidha Waziri wa kilimo Mheshimiwa Bashe ameahidi kuyafutia leseni makampuni ya mbegu yatakayokwenda kinyume na maelekezo na maagizo kuhusu bei elekezi ya bei za jumla na bei ya rejareja baada ya kutangazwa siku hiyo ya tarehe 20 oktoba, pia ameyaasa makampuni ya mbegu kuhakiksha yanatoa kwenye magazeti bei elekezi kama walivyokubaliana.

Hata hivyo katika kuhakikisha utekelezaji wa suala hili Waziri Bashe amesema Serikali kupitia Wizara ya kilimo itatoa vibali kwa wakuu wa wilaya kutembelea maduka ya uuzaji wa mbegu kuhakiki utekelezaji wa agizo hilo na kuchukua hatua za kuyafunga maduka yote yatakayokwenda kinyume na agizo hilo.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI