Na Deus Kibamba
Tukiwa tayari tuko mwishoni mwa mwaka 2023, sasa ni dhahiri kuwa haiwezekani kukamilisha Mchakato wa Katiba Mpya na kuanza kuitumia Katiba Mpya kabla ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024 au Uchaguzi Mkuu 2025.
Kitaalamu, katika hatua hii tuliyopo, yapo mambo kadhaa tunaweza kuyafanya kama nchi ili kuepuka hali ya taharuki huko tuendako. Moja ni kuuahirisha rasmi mchakato huo ili tuendelee nao baada ya Uchaguzi Mkuu 2025.
Pili ni kuboresha sheria mbalimbali zinazogusa masuala ya uchaguzi ili Uchaguzi Mkuu ujao usifanyike ukiwa na malalamiko yaleyale ya miaka nenda, miaka rudi.
Kama taifa, tunapaswa tufanye juhudi za kuunasua Mchakato wa Katiba Mpya kutoka topeni kichakani, tuuache ukiwa mahali pazuri na peupe.
Mwisho
0 Comments