Header Ads Widget

TPA YAFUNGUA OFISI ZIMBABWE

 

WAZIRI wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (katikati) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi na Maendeleo ya Miundombinu Nchini Zimbabwe  Joy Makumbe (wa pili kushoto ), wakikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa Ofisi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania  (TPA) Jijini Harare Zimbabwe, tarehe 16 Oktoba, 2023.

Wengine katika picha ni Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. Simon Sirro ( kushoto) na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Juma Kijavara ( kulia)

Na Mwandishi Wetu


SERIKALI imesema uhusiano wa Tanzania na Zimbabwe katika sekta za biashara na uchukuzi utaendelea kuwaimarishwa baada ya kufanyakazi kwa pamoja ili kupata ufumbuzi wa kero na changamoto zinazokwamisha kasi ya kukua kwa biashara katika ushoroba wa Dar es Salaam.

Maazimio hayo yalifikiwa Oktoba 16, 2023 kati ya Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Zimbabwe, Mhandisi Joy Makumbe kuthibitisha Nia ya serikali zao kuimarisha uhusiano wa kihistoria.

Aidha, wawakilishi hao wa Serikali hizo, walifikia maamuzi hayo wakati wa hafla ya ufunguzi wa ofisi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), mjini Harare, nchini Zimbabwe.

"Tanzania na Zimbabwe inatumia fursa za kiuchumi zilizopo katika pande zote mbili kwa manufaa ya wananchi wetu" alisema Profesa Mbarawa.


Mwisho 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI