Header Ads Widget

VIJIJI 16 RUANGWA KUINGIZWA KWENYE MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI

 



NA HADIJA OMARY 



LINDI.......Jumla ya vijiji 16 vya halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi vinatarajiwa kuingizwa kwenye mpango wa Matumizi bora ya Aridhi 


Hayo yameelezwa na Afisa Mipango Miji na Vijiji Kutoka tume ya taifa ya Mipango ya Matumizi ya ardhi Fadhili Makame Wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji Cha Chikwale halmashauri ya wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi 



Mkutano huo ulilenga  kutambulisha mradi wa Mpango huo wa Matumizi ya Ardhi kwenye kijiji hicho ambapo  amesema kupitia mpango huo Kwa awamu ya kwanza unatarajia kuhusisha Vijiji nane.



Mpango wa Matumizi ya Ardhi katika wilaya ya Ruangwa unawezeshwa na tume ya taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi Kwa kushirikiana na Halmashauri ya wilaya ya Ruangwa



Makame amesema vijiji hivyo  ni Chiundu, Chikwale, Namkatile, Nandandala, Namkonjela, Mkaranga, Nambilanje na Nanjaru



Aidha alisema kuwa awamu ya pili vitahusika vijiji vya Namkatila , Nandandala, Namkonjela,  mkaranga, Nambilanje,  Nanjaru, Chiundu, Chikwale,  Nangaru, Mchecha , Nandanga , Likwachu, Litama, Mibule , Chilangalile na Chikoko



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI