Header Ads Widget

MICHAEL MLOWE SI MTALII TANZANIA – UHAMIAJI

 

Kamishna wa Paspoti na Uraia Gerald Kihinga  ni Kamishna wa Paspoti na Uraia

MAYKO Jaess Namlowe (Michael Mlowe) sio mtalii ni mharifu  wa makosa ya  jinai  hii ni kauli ya Ofisi ya  uhamiaji Taifa iliyotolewa   kwa  waandishi  wa habari .


Kumekuwepo na mijadala  mbali mbali  kwenye vyombo  vya habari  vya mtandaoni  hususani makundi ya  WhatSApp juu ya  taarifa  za  kukamatwa  kwa muingereza   huyu mwenye  asili ya Tanzania mzaliwa  wa  mkoa wa Iringa .


Kutokana na  Sintofahamu   hiyo   timu ya  matukio Daima  media  imelazimika  kufunga  safari   kutoka mkoani Iringa Zaidi ya  kilomita  500 hadi jijini Dar es Salaam  ofisi za Uhamiaji  Taifa  ili  kupata  ukweli  wa  sakata  hili.



Kamishna wa Paspoti na Uraia Gerald Kihinga  ni Kamishna wa Paspoti na Uraia anakutana na  timu ya  waandishi wa habari  kwa  niaba ya kamishna mkuu wa Uhamiaji   Taifa Anna Makakala ambae kwa  wakati  huo alikuwa nje ya  jiji la Dar es Salaam kwa majukumu ya  kikazi .

 

Kihinga  alisema Mlowe  ambae anafahamika kama Namlowe ni kweli anashikiliwa uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere kwa kutaka  kuingia nchini bila kibali  cha waziri  wa mambo ya ndani ya nchi.

“Namlowe alipoteza sifa ya kuwa Mtanzania baada ya kwenda nchini Uingereza na kupata paspoti ya nchi hiyo yenye namba GBR- 562745957 inayokwisha muda wake Oktoba 10, 2029” alisema

Kamishna Kihinga alisema Mlowe amekuwa na tuhuma nyingi za kiuhamiaji pamoja na  makosa mbalimbali ya kijinai kama vile kughushi nyaraka  za serikali na kuwatukana viongozi wa serikali kwenye mitandao ya kijamii na kujishughurisha na siasa wakati yeye si raia wa Tanzania.

Anaendelea kusema kuwa mwaka 2018 Mlowe alifikishwa Mahakamani kwa kosa la kumiliki paspoti mbili, kughushi nyaraka, kujihusisha na siasa na kwamba alikiri makossa kwenye kesi namba 306 ya mwaka 2018 katika Mahakama ya Kisutu na alihukumiwa kifungo au faini ya shilingi 630,000.

“Mlowe alilipa faini hiyo hivyo kwa kuwa yeye ni raia wa nje alikiri makossa Makahamani tukamuondosha nchini kwa sababu anatuvurugi amani ya nchi yetu kwa hiyo alirudi kwao Uingereza,

Sasa tukashangaa tarehe 30 Agosti 2023 kupitia shirika la ndege la Ujerumani (KLM) namba KLM 569kupitia uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere alirejea nchini. Hivyo tumemuamuru arudi nchini kwao hatutaki vurugu katika nchi yetu”. Alisema Kamishna Kihinga.

Kamishna Kihinga alisema mtu akishakuwa na makosa ya jinai  uwezi kumruhusu kuingia nchini bali nchi ndiyo yenye mamlaka ya kumruhusu aingie au asiingie hata hivyo amepewa taratibu kama anataka kuingia ni lazima aombe kibari kwa Waziri wa  Mambo ya Ndani lakini siyo yeye kufanya fujo ya kulazimisha aingie sharia hairuhusu.

“Kwa  sasa yupo uwanja wa ndenge amezuiliwa kuingia nchini lakini kunakitu alighushi katika mifumo yetu tuliweza kumzuia alichokifanya alikwenda kubadilisha sehemu ya kuzaliwa alisema kazaliwa Burundi na siyo Tanzania kwa hiyo baada ya kubaini yote haya hatuwezi kumruhusu kuingia huyo ni mharifu wa Kimataifa”. Alisema Kamishna Kihinga.

Akizungumzia suala la kwamba Mlowe ni moja kati ya watalii walioitikia wito kupitia jitihada  za  Rais  Dkt  Samia Suluhu Hassan kwa  kuzunguka kutangaza  utalii  kupitia filamu ya Royal Tour ,Kamishna Kihinga alisema huyo siyo mtalii kwani mtalii aghushi nyaraka huyo ni mharifu wa makossa ya jinai hatakiwi nchini.

Hata hivyo alivyoulizwa kuhusu Uhamiaji kutumika vibaya kwa kutumiwa kuingiza masuala ya idara hiyo na masuala binafsi ya ugomvi wa kifamilia kati yake na mzazi mwenzake ofisa huyo alisema si kweli Uhamiaji inafanya kazi yake kwa mujibu wa sharia na si vinginevyo.

Kukamatwa kwa Michael Mlowe kumekuwepo na mijadara mbalimbali katika mitandao ya kijamii wakimshutumu Kamishna Mkuu wa Uhamiaji nchini Anna Makakala kutumika kumkandamiza Mlowe kupitia ofisi ya uhamiaji, katika moja ya kauli yake Michaele Mlowe kwenye mitandao ya kijamii alinukuliwa akisema hana ugomvi na mzazi mwenzake wala ofisi ya uhamiaji anaheshimu taifa lake Tanzania na wala hana ugomvi na idara ya usalama wa Taifa.

“Mimi sina ugomvi na mzazi mwenzangu, ofisi ya Uhamiaji wala Idara ya Usalama wa Taifa naiheshimu nchi yangu Tanzania”. Alisema Mlowe.

Jitiahda  za  kumtafuta  waziri wa  mambo ya  ndani ya nchi  Mhandisi  Hamad Masauni bado zinafanyika  ili  kujua hatima  ya Namlowe kutembelea nchi ya  Tanzania  endelea kufuatilia undani wa sakata  hili.

PAKUA APP YA MATUKIO DAIMA AMA TEMBELEA CHANEL YA MATUKIO DAIMA TV KUONA VIDEO NZIMA 

  

 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI