Header Ads Widget

TOSCI YAFANIKIWA KUDHIBITI TATIZO LA UZALISHAJI MBEGU FEKI

 


Na Hamida Ramadhan Matukio Daima APP DODOMA


TAASISI ya uthibiti  ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) imesema imeweza kudhibiti tatizo la uzalishaji Mbegu feki hapa nchini kwa lengo la kuhakikisha kuwa na mazao yenye tija ikiwa ni pamoja na kuwafikisha Mahakamani watu ambao walijihusisha na uzalishaji wa Mbegu feki. 


Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi  hiyo,PATRICK NGWEDIAGI ameyaeleza hayo Jijini Dodoma  wakati akitoa Taarifa mbele ya Waandishi wa Habari kuhusu  utekelezaji wa Majukumu ya TOSCI na mwelekeo wa utekelezaji kwa Mwaka wa Fedha  2023/2024.


" Kama taasisi tumeweza kudhibiti tatizo la uzalishaji mbegu feki hapa nchini na lengo letu lilikuwa kumpatia mkulima mbegu bora na kuleta tija kwenye mazao," Amesema NGWEDIAGI.


Pamoja na hayo,NGWEDIAGI amebainisha kuwa  kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 Taasisi ya TOSCI,inatarajia kutumia jumla ya Shilingi Bilioni12.6kwaajili ya kutekeleza  Mradi wa Sekta ya Kilimo na Uvuvi ikiwemo Kujenga Maabara kubwa ya kisasa ambayo itaweza kuchambua na kupima ubora wa Mbegu.


Katika hatua nyingine,Mkurugenzi Mkuu huyo amesema kutokana na Mbegu zinazozalishwa kuzingatia  ubora, jumla ya Tani elfu nne,zimeuzwa nje ya Nchi.


Taasisi ya uthibiti ubora wa Mbegu Tanzania hivi sasa imeweza kuongeza ufanisi wa uzalishaji Mbegu zenye ubora kwa asilimia 75 Toka asilimia 35 ambapo ni ongezeko kubwa.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI