Header Ads Widget

RAIS DKT. MWINYI AWASISITIZA WADAU KUSIMAMIA NA KULINDA RASILIMALI YA MAJI CHINI YA ARDHI

 


NA THABIT MADAI,ZANZIBAR - MATUKIO DAIMA APP


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt HusseinAli Mwinyi amesisitiza Wadau katika Sekta ya Maji  kuendelea kusimamia ipasavyo rasilimali ya maji chini ya Ardhi ili kukabiliana na athari ya Mabadiliko ya Tabia nchi ambayo yanazidi kuongezeka Nchini.



Rais Dkt Hussein Ali Mwinyi ametoa Wito huo leo wakati akifungua Kongamano la Pili la Kimataifa la Maji lililifanyika ukumbi wa Hotel Verde Mtoni Marine Mjini  Magharib Unguja.



Amesema kuwa, Zanzibar bado inachangamoto ya vyanzo vingi vya Maji na inategemea Maji chini ya Ardhi hivyo Wadau wanapaswa kulinda miundombinu ya maji na kuvilinda vyanzo vya maji vilivyopo kwa kuviepusha na shughuli zao zikiwemo ujenzi na kuanzisha makazi.



Aidha, aliitaka jamii kuendelea kuimarisha mazingira kwa kupanda miti ambayo ni muhimu kwa upatikanaji wa mvua.



Pia, Dk. Mwinyi aliwaagiza viongozi wa Wizara ya Maji, Nishati na Madini, kuhakikisha wanafanya kazi kwa karibu na watafiti wanaofanya utafiti kwenye sekta hiyo, ili wawe na mipango madhubuti ya kukusanya na kutumia matokeo ya utafiti unaofanywa Zanzibar kwa maendeleo ya taifa.



Halikadhalika aliutaka uongozi wa Wizara hiyo, kuandaa mpango wa muda mrefu wa Sekta ya Maji ili usaidie kubainisha miongozo ya sekta hiyo na hatimae kupunguza changamoto zilizopo.



Vilevile, Dk. Mwinyi aliutaka uongozi wa Wizara hiyo kushirikiana na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makaazi, kuandaa utaratibu wa kuyatambua na kuyapatia hatimiliki maeneo yote ya vyanzo vya maji, Zanzibar.



Alisema, Serikali itaendelea kuimarisha sekta ya maji kwa kutekeleza miradi mikubwa kama ilivyopangwa na kuelekezwa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi na Dira ya Maendeleo ya Zanzibar 2050, kufuatia ahadi alizozitoa wakati wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2020.



Pia, alieleza miradi mikubwa ya maji inayoendelezwa za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia fedha za Mkopo wa Ahueni ya UVIKO kutoka shirika la Fedha duniani (IMF) itatoa mchango mkubwa na kuondoa changamoto za maji zilizopo kwenye maeneo mbalimbali ya Unguja na Pemba.




Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Maji wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Juma Aweso, Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Maryprisca Mahundi alieleza Serikali ya SMT kupitia Wizara aiko hatua za mwisho za maangali ya miradi yake mikupwa ya mumtua ndoo ya maji mama kichwani.




Naye, Waziri wa Maji Nishati na Madini, Shaibu Hassan Kaduara, aleleza nia ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika jitihada zake za kuwafikishia wananchi huduma za maji safi na salama nakueleza mwezi Septemba mwaka huu Serikali kwa mara ya kwanza inatarajia kuzindua nangi la maji la lita milioni 32, ambayo litasambaza maji kwenye maeneo mengi ya Zanzibar.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI