Na Jusline Marco-Matukio Daima App, Arusha.
Kampuni ya Agricom katika maoneshoya Nanenane njiro jijini Arusha imetambulisha zana mpya ya kilimo aina ya KUBOTA yenye nguvu 75 ambayo ina fouwill na toowill kwa mara moja ambayo inatofauyishwa na trekta nyinngine ambazo zipo sokoni.
Akizungumza katika banda la Agricom Afrika kwenye maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini jijini Arusha Meneja wa Kanda ya Kati na Kaskazini Peter Temu,amesema uwezo wa trekta hiyo ni sawa na uwezo wa kutumia trekta mbili kwa mara moja ambayo inauwezo wa kufanya kazi mahali popote kilingana na aina ya udogo.
Ameongeza kuwa matengemeo yao ni kuwasaidia wakulima wa Kanda ya Kaskazini wawe kufanya vizuri kwenye kilimo chao ukitengemea treka hho pamoja na kuwa na nhuvu ya 75 ina ubora mkubwa kwenye matumizi ya mafuta ,bei inayouzwa hadi katika upatikanaji wa vipuri .
Pichani: Peter Temu Meneja wa Kanda ya Kati na Kaskazini kutoka kampuni ya Agricom Afrika kwenye maonesho ya Nanenane Kanda ya Kaskazini jijini Arusha.
Vilevile Meneja huyo amewataka wakulima kutarajia kupata kutokana na kile wanachokifanya kutokana na kwamba teknolojia hiyo niya japani inayosambazwa na Agricom Afrika ambapo pia hutathimini njia ya kumuwezesha mkulima aweze kupata faida zaidi kwa kumuinua kutoka katika matumizi ya zana za zamani na kurudi katika matumizi ya zana za kisasa zinazomuwezesha mkulima kupata faida kutokana na kile anachokifanya.
Awali akigungua maonesho hayo Spika wa bunge la Baraza la wawakilishi Zanzibar Mhe. Zuberi Ali Maulidi amesema kwa kipindi chwa 2022/23 serikalk ya Tanzania iliweka nguvu kubwa kwenye katika kuboresha kilimo na mifugo ambapo mikoa ya kanda ya kaskazini imenufaika na mamno mbalimbali ikiwemo utolewaji wa mnolea za ruzuku kwa ajili ya kuongeza tija kwenye kilimo.
Aidha Mhe.Maulidi amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/23 jumla ya Tani 17288 zimetolewa kwa mkoa wa Arusha na kuwanufaisha wakulima 19663 na Tani 18557 zimetolewa kwa mkoa wa Kilimanjaro na kuwanufaisha wakulima 62829 huku Mkoa wa Manyara ukipata Tani 4840 na kinufaisha wakilima 6829.
Vilevile amewataka wananchi kuendelea kutoa ushirikiako kwa serikali ili iweze kuendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ambapk amesema maonesho hayo yana lenho la kuonyesha fursa zilizopo katika sekta za kilimo,mifugo na uvuvi na kutoa elimu kwa wakulima,wafugaji na wavuvi ili uzalishaji wa mazao na bidhaa zinazotokana na sekta hizo uwe na tija na hatimaye kuchangia katika ukuaji wa uchumi wa nchi.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongela amesema kuwa maonyesho ya wakulima nanenane yamezidi kuimarika na kuleta chachu katika sekta mbalimbali hivyo ushirikiano wa kimuungano utaendelea kuleta chachu zaidi Kwa wananchi wote wa Tanzania bara na visiwani.







0 Comments