Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)nchini wameshauriwa kufanya kazi kwa juhudi na kuimarisha uchumi wao ili kuepuka utegemezi unaoweza sababisha vijana hao kutumika vibaya katika nyanja ya kisiasa.
Hayo yamesemwa na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa, Mhe Ritta Kabati wakati alipokuwa akiongea na vijana wa Chama Cha Mapinduzi katika ofisi za UVCCM wilaya ya Iringa Vijijini.
Katika hatua nyingine, Mh Kabati amesema vijana wa Chama Cha Mapinduzi wanapaswa kusema kazi nzuri zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita ya Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo kwa Watanzania.
0 Comments