Header Ads Widget

FIDIA ZA LIGANGA NA MCHUCHUMA LUDEWA NJOMBE KULIPWA JUNI 7,2023

 



Na Gabriel Kilamlya Matukio DaimaAPP NJOMBE 


Jumla ya Watu  1142 wanatarajiwa kuanza kulipwa fidia  za kupisha maeneo ya madini ya Chuma na Makaa  ya mawe Wilayani Ludewa mkoani Njombe hapo Juni 7 mwaka huu kiasi Cha  zaidi  shilingi bilioni  15.4.


Mkurugenzi mtendaji wa Shirika la maendeleo la taifa NDC Dkt Nicolaus Shombe  amesema tayari uhakiki wote ulishafanyika na wanufaika walishakula kiapo hivyo zoezi hilo litazinduliwa rasmi siku ya juma tano ya wiki hii.


Amesema kutakuwepo na shughuli mbalimbali ndani ya miradi hiyo kikiwemo chuo Cha ufundi na hivyo mwakani shughuli za uchimbaji migodi hiyo inatarajiea kuanza.



Mkuu wa mkoa wa Njombe Antony Mtaka amesema uzinduzi huo utafanyika na waziri wa viwanda biashara na uwekezaji Dkt.Ashatu Kijaji zoezi litakalofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Ludewa.


Aidha Mtaka amesema fedha hizo pia zinaweza kuwasaidia kuwekeza katika shughuli nyingine badala ya kwenda kuzitumia vibaya.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS